Skip to main content

Sakata la vyeti feki lazua mjadala

Wasomi wamepinga kufanyika kwa ubaguzi wa wenye vyeti feki kwa kuwaacha baadhi ya mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya katika uhakiki huo.

Kauli hiyo imekuja siku moja  baada ya Rais John Magufuli kuagiza wafanyakazi 9,932 waliobainika kuwa na vyeti feki, waondolewe kazini.

Uamuzi huo wa Serikali umesaidia kunusuru kutumika kwa fedha nyingi kuwalipa watu wasiokuwa na sifa.

Kama watumishi hao wote wanalipwa kiwango cha kima cha chini cha mshahara cha Sh300,000 jumla ya Sh35.7 bilioni zimekuwa zikitumika kila mwaka kuwalipa.

Wakati akikabidhi orodha hiyo juzi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah  Kairuki amesema kazi hiyo haikuwagusa mawaziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kwa kuwa wao wanatakiwa kujua kusoma na kuandika.

Kauli hiyo imeibua mjadala mzito kwa kile kilichodaiwa inalenga kutetea uovu na kuhalalisha  mambo yasiyofaa bila kuangalia wakati uliopo.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM), Bashiru Ally amesema licha ya kuwa kauli ya Kairuki ilitolewa kisheria lakini wakati umefika sasa kwa kuangaliwa upya kwa sheria hiyo ili watumishi wa Serikali wanaopatikana kisiasa nao wawe na elimu ya kutosha.

Amesema kwa waziri ambaye anasimamia masuala mbalimbali na kuwaongoza watu wengi walio chini yake ni kichekesho na aibu kueleza kuwa sifa kubwa anayotakiwa kuwa nayo ni kujua kusoma na kuandika.

Hoja hiyo pia imeungwa mkono na Profesa Gaudence Mpangala wa Chuo Kikuu cha Ruaha ambaye amesisitiza ipo haja ya kuangaliwa upya kwa suala hilo kwani kuruhusiwa wanasiasa kuwa na vyeti feki ni hatari zaidi.     Chanzo Cha Habari: muungwana.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...

Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi

Hii Ndiyo Tafsiri sahihi Ya Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi Moja ya kitu ambacho huwa hakina kipaumbele sana katika mahusiano ya kimapenzi,  kitu ambacho kinachoitwa zawadi. Lakini ukweli ni kwamba zawadi ina maana kubwa sana katika mahusiano ya kimapenzi zaidi hata udhaniavyo. Na Katika tafiti ambazo zimewahi fanywa ni kwamba, suala zima la utoaji zawadi katika mahusiano ya kimapenzi lilimekuwa likileta hisia zaidi katika upande mmoja. Yaani hapa nikiwa na maana ya kwamba jinsia ya kike ndiyo ambayo ipo katika kusubiri zawadi kutoka kwa jinsia ya kiume. Kutoka na suala hilo ndo maana watu wengi wamekuwa hawatilii maanani suala zima la zawadi. Lakini ukweli ni kwamba kila mtu anahusika kutoa zawadi. Huenda ukawa bado nakuacha njia panda huelewi ni zawadi gani ambayo itampendeza mpenzi wako. Wala usipate tabu afisa Mipango nipo kwa ajili yako. Ipo hivi ili kujua zawadi ambayo mwezi wako anapendezwa nayo,  Unachotakiwa kukifanya ni kwamba kwa kuwa ni mpen...