Skip to main content

Hasira zetu kwa Mbao

Mkude asema hasira zetu tutazishusha kwa Mbao



NAHODHA WA SIMBA, JONAS MKUDE.

NAHODHA wa Simba, Jonas Mkude, amesema kuwa hasira za kupotez a mchezo wao dhidi ya Kagera Sugar wanazitua kesho kutwa kwenye mchezo wao dhidi ya Mbao FC.

Simba itakuwa mgeni wa MbaoFC kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ukiwa ni mchezo wa pili wa timu hiyo kanda ya Ziwa.

Akizungumza na gazeti hili jana muda mfupi kabla ya kuanza kwa mazoezi ya timu hiyo, Mkude, alisema kuwa imewauma sana kupoteza mchezo wao na kagera Sugar uliowapelekea kutolewa kwenye kiti cha uongozi wa ligi na sasa wanataka kusahau hayo kwa kushinda mchezo wao wa Jumatatu.

"Bado kwenye nafsi zetu kuna kitu kinatuuma baada ya kupoteza mchezo wetu kule Bukoba.., ili kusahau yote tunapaswa kushinda kwenye mchezo unaofuata dhidi ya Mbao.., tumejipanga kuhakikisha tunashinda mchezo huu ili kurudisha furaha ya mashabiki wetu," alisema Mkude.

Aidha, alisema mbali na mchezo huo, pia wanataka kuhakikisha wanaondoka na pointi tatu kwenye mchezo dhidi ya Toto African utakaochezwa siku nne baada ya mchezo huo wa Jumatatu.

"Lengo letu likuwa kuondoka hukuKanda ya Ziwa na pointi zote tisa, lakini kwa bahati mbaya tumepoteza pointi tatu..., tutahakikisha hizi sita zilizobakia tunaondoka nazo,"aliongeza kusema Mkude.

Aidha, alisema mashabiki wa timuhiyo kuwa na umoja na kuendelea kuiunga mkono timu yao kwa kuwa bado ipo kwenye mbio za kuwania ubingwa.

"Pamoja na kufungwa na Kagera, bado tupokwenye mbio za ubingwa na tunaweza tukatimiza malengo yetu.., bado tuna michezo mingine mbele yetu na tumekuwa na utofauti mdogo wa pointi na timu inayoongoza ligi," alisema Mkude.

Simba inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 55 ikizidiwa kwa pointi moja na Yanga inayoongoza ligi. 
Habari kutoka muungwana blog.


Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta...

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as...

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...