Skip to main content

Hasira zetu kwa Mbao

Mkude asema hasira zetu tutazishusha kwa Mbao



NAHODHA WA SIMBA, JONAS MKUDE.

NAHODHA wa Simba, Jonas Mkude, amesema kuwa hasira za kupotez a mchezo wao dhidi ya Kagera Sugar wanazitua kesho kutwa kwenye mchezo wao dhidi ya Mbao FC.

Simba itakuwa mgeni wa MbaoFC kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ukiwa ni mchezo wa pili wa timu hiyo kanda ya Ziwa.

Akizungumza na gazeti hili jana muda mfupi kabla ya kuanza kwa mazoezi ya timu hiyo, Mkude, alisema kuwa imewauma sana kupoteza mchezo wao na kagera Sugar uliowapelekea kutolewa kwenye kiti cha uongozi wa ligi na sasa wanataka kusahau hayo kwa kushinda mchezo wao wa Jumatatu.

"Bado kwenye nafsi zetu kuna kitu kinatuuma baada ya kupoteza mchezo wetu kule Bukoba.., ili kusahau yote tunapaswa kushinda kwenye mchezo unaofuata dhidi ya Mbao.., tumejipanga kuhakikisha tunashinda mchezo huu ili kurudisha furaha ya mashabiki wetu," alisema Mkude.

Aidha, alisema mbali na mchezo huo, pia wanataka kuhakikisha wanaondoka na pointi tatu kwenye mchezo dhidi ya Toto African utakaochezwa siku nne baada ya mchezo huo wa Jumatatu.

"Lengo letu likuwa kuondoka hukuKanda ya Ziwa na pointi zote tisa, lakini kwa bahati mbaya tumepoteza pointi tatu..., tutahakikisha hizi sita zilizobakia tunaondoka nazo,"aliongeza kusema Mkude.

Aidha, alisema mashabiki wa timuhiyo kuwa na umoja na kuendelea kuiunga mkono timu yao kwa kuwa bado ipo kwenye mbio za kuwania ubingwa.

"Pamoja na kufungwa na Kagera, bado tupokwenye mbio za ubingwa na tunaweza tukatimiza malengo yetu.., bado tuna michezo mingine mbele yetu na tumekuwa na utofauti mdogo wa pointi na timu inayoongoza ligi," alisema Mkude.

Simba inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 55 ikizidiwa kwa pointi moja na Yanga inayoongoza ligi. 
Habari kutoka muungwana blog.


Comments

Popular posts from this blog

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta...