Skip to main content

Kompyuta yampeleka jela miaka 4

Kompyuta yampeleka jela miaka 4

MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala, imemhukumu kwenda jela kutumikia kifungo cha miaka minne mkazi  wa Dar es Salaam, Ramadhani Hatibu (30), maarufu kama  Mbishi,  baada ya kukutwa na  hatia kwa wizi wa kompyuta mpakato (laptop) yenye thamani ya Sh.  milioni 1.3.

Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi, Catherine Kiyoja.

Hakimu alisema baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na pande zote mbili, mahakama imemuona mshtakiwa ana hatia na kwamba inamhukumu kwenda jela bila kuacha shaka.

Mbali na kifungo hicho,  mahakama imemtaka mshtakiwa kumlipa mlalamikaji, Edger Mahundi,  faini ya Sh. milioni 1.5  baada ya kumaliza kutumikia adhabu.

Akisoma hukumu hiyo,  Hakimu  Catherine  alisema ameridhishwa na ushahidi wa mashahidi wanne ambao walithibitisha shtaka  pasi kuacha shaka yoyote.

“Mshitakiwa ninakutia hatiani,  utatumikia kifungo cha miaka minne jela na ukitoka jela unatakiwa kumlipa Mahundi faini ya Sh. milioni 1.5,” alisema.

Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo,  Wakili wa Serikali, Florida Wenceslaus, aliomba mahakama impe adhabu kali mshtakiwa kwa sababu kitendo cha kuingia ndani ya nyumba na kuiba ni cha ovu, hivyo apewe adhabu kali ili iwe fundisho kwake na wengine.

Hata hivyo, mahakama ilitoa nafasi kwa mshtakiwa kujieleza na aliomba apunguziwe adhabu akidai ni kosa lake la kwanza na ana wategemezi wakiwamo mke, watoto wawili na mama yake mzazi ambaye ni mgonjwa.

Mshtakiwa huyo anadaiwa kutenda kosa hilo,  Septemba 8, 2015 katika eneo la Ulongoni B Wilaya ya Ilala.

Inadaiwa siku hiyo,  aliiba kompyuta hiyo moja yenye thamani ya Sh. milioni  1.3, mali ya Mahundi.

Comments

Popular posts from this blog

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta...