Skip to main content

Kompyuta yampeleka jela miaka 4

Kompyuta yampeleka jela miaka 4

MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala, imemhukumu kwenda jela kutumikia kifungo cha miaka minne mkazi  wa Dar es Salaam, Ramadhani Hatibu (30), maarufu kama  Mbishi,  baada ya kukutwa na  hatia kwa wizi wa kompyuta mpakato (laptop) yenye thamani ya Sh.  milioni 1.3.

Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi, Catherine Kiyoja.

Hakimu alisema baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na pande zote mbili, mahakama imemuona mshtakiwa ana hatia na kwamba inamhukumu kwenda jela bila kuacha shaka.

Mbali na kifungo hicho,  mahakama imemtaka mshtakiwa kumlipa mlalamikaji, Edger Mahundi,  faini ya Sh. milioni 1.5  baada ya kumaliza kutumikia adhabu.

Akisoma hukumu hiyo,  Hakimu  Catherine  alisema ameridhishwa na ushahidi wa mashahidi wanne ambao walithibitisha shtaka  pasi kuacha shaka yoyote.

“Mshitakiwa ninakutia hatiani,  utatumikia kifungo cha miaka minne jela na ukitoka jela unatakiwa kumlipa Mahundi faini ya Sh. milioni 1.5,” alisema.

Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo,  Wakili wa Serikali, Florida Wenceslaus, aliomba mahakama impe adhabu kali mshtakiwa kwa sababu kitendo cha kuingia ndani ya nyumba na kuiba ni cha ovu, hivyo apewe adhabu kali ili iwe fundisho kwake na wengine.

Hata hivyo, mahakama ilitoa nafasi kwa mshtakiwa kujieleza na aliomba apunguziwe adhabu akidai ni kosa lake la kwanza na ana wategemezi wakiwamo mke, watoto wawili na mama yake mzazi ambaye ni mgonjwa.

Mshtakiwa huyo anadaiwa kutenda kosa hilo,  Septemba 8, 2015 katika eneo la Ulongoni B Wilaya ya Ilala.

Inadaiwa siku hiyo,  aliiba kompyuta hiyo moja yenye thamani ya Sh. milioni  1.3, mali ya Mahundi.

Comments

Popular posts from this blog

je wajua,zifahamu mbinu mbalimbali za kumpata mwenzi bora

KILA mtu anapenda kuwa na mwenza mzuri, mwenye kumfaa katika maisha yake. Hata hivyo kwa bahati mbaya ni kwamba wengi wanashindwa kupata wenza wazuri. Ziko sababu nyingi lakini kubwa ni uwezo wa mtu wa kumtambua mwingine na kujua kama ni kweli anafaa au anafaa  kuendana nae au la.Wakati wa uchumba, wengi wa watu huonekana kutumiana kadi, zawadi na mambo mengine  mbalimbali yenye lengo la kuonyesha wanapendana. Aidha, wapo ambao wanashindwa kujua namna ya kutongoza; kwa ujumla kutongoza ni uwezo wa ushawishi kwamba unamwambia mwanamke unamuhitaji na kumpenda awe wako au wakati mwingine hata mwanamke anaweza kuanza. Ndio ukweli wenyewe Sio kweli kwamba kila mwanaume anajua kutongoza. Kuna wengine hata kumsimamisha mwanamke hawezi au anaogopa. Ndio unaweza kukuta mwanamume anajikanyaga namna ya kuongea. Wapo wengine wanafikiri njia sahihi ya kutongoza ni kuhonga aidha fedha au mali nk, lakini sicho hasa wanachotaka wanawake au wanaume katika mapenzi. Maneno ya ku...

Aliyoyajibu Lulu Diva baada ya kudaiwa kuwa mapenzini na Madee

Aliyoyajibu Lulu Diva baada ya kudaiwa kuwa mapenzini na Madee April 6, 2017 kupitia U heard ya XXL ya Clouds FM staa wa Bongo Fleva Lulu Diva ameweka wazi uhusiano wake na staa mwingine wa Bongo Fleva kutoka Tip Top Connection,   Madee baada ya kuonekana mara kwa mara wakiwa pamoja. Soudy Brown aliwatafuta Madee na Lulu Diva kufahamu ukweli ambapo Madee hakupatikana kwenye simu, lakini Lulu Diva alikuwa na haya ya kujibu alipoulizwa kuhusu kutoka kimapenzi na Madee . ..>>> “Madee ni kaka yangu na nimshauri wangu halafu pia kuna wimbo wake amenishirikisha, Soudy na wewe umezidi umbea, T-shirt akivaa Madee sisi wengine hatuwezi kununua? T-shirt tumenunua sare, tumenunua siku moja.”  – Lulu Diva.

Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi

Hii Ndiyo Tafsiri sahihi Ya Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi Moja ya kitu ambacho huwa hakina kipaumbele sana katika mahusiano ya kimapenzi,  kitu ambacho kinachoitwa zawadi. Lakini ukweli ni kwamba zawadi ina maana kubwa sana katika mahusiano ya kimapenzi zaidi hata udhaniavyo. Na Katika tafiti ambazo zimewahi fanywa ni kwamba, suala zima la utoaji zawadi katika mahusiano ya kimapenzi lilimekuwa likileta hisia zaidi katika upande mmoja. Yaani hapa nikiwa na maana ya kwamba jinsia ya kike ndiyo ambayo ipo katika kusubiri zawadi kutoka kwa jinsia ya kiume. Kutoka na suala hilo ndo maana watu wengi wamekuwa hawatilii maanani suala zima la zawadi. Lakini ukweli ni kwamba kila mtu anahusika kutoa zawadi. Huenda ukawa bado nakuacha njia panda huelewi ni zawadi gani ambayo itampendeza mpenzi wako. Wala usipate tabu afisa Mipango nipo kwa ajili yako. Ipo hivi ili kujua zawadi ambayo mwezi wako anapendezwa nayo,  Unachotakiwa kukifanya ni kwamba kwa kuwa ni mpen...