Skip to main content

Kompyuta yampeleka jela miaka 4

Kompyuta yampeleka jela miaka 4

MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala, imemhukumu kwenda jela kutumikia kifungo cha miaka minne mkazi  wa Dar es Salaam, Ramadhani Hatibu (30), maarufu kama  Mbishi,  baada ya kukutwa na  hatia kwa wizi wa kompyuta mpakato (laptop) yenye thamani ya Sh.  milioni 1.3.

Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi, Catherine Kiyoja.

Hakimu alisema baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na pande zote mbili, mahakama imemuona mshtakiwa ana hatia na kwamba inamhukumu kwenda jela bila kuacha shaka.

Mbali na kifungo hicho,  mahakama imemtaka mshtakiwa kumlipa mlalamikaji, Edger Mahundi,  faini ya Sh. milioni 1.5  baada ya kumaliza kutumikia adhabu.

Akisoma hukumu hiyo,  Hakimu  Catherine  alisema ameridhishwa na ushahidi wa mashahidi wanne ambao walithibitisha shtaka  pasi kuacha shaka yoyote.

“Mshitakiwa ninakutia hatiani,  utatumikia kifungo cha miaka minne jela na ukitoka jela unatakiwa kumlipa Mahundi faini ya Sh. milioni 1.5,” alisema.

Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo,  Wakili wa Serikali, Florida Wenceslaus, aliomba mahakama impe adhabu kali mshtakiwa kwa sababu kitendo cha kuingia ndani ya nyumba na kuiba ni cha ovu, hivyo apewe adhabu kali ili iwe fundisho kwake na wengine.

Hata hivyo, mahakama ilitoa nafasi kwa mshtakiwa kujieleza na aliomba apunguziwe adhabu akidai ni kosa lake la kwanza na ana wategemezi wakiwamo mke, watoto wawili na mama yake mzazi ambaye ni mgonjwa.

Mshtakiwa huyo anadaiwa kutenda kosa hilo,  Septemba 8, 2015 katika eneo la Ulongoni B Wilaya ya Ilala.

Inadaiwa siku hiyo,  aliiba kompyuta hiyo moja yenye thamani ya Sh. milioni  1.3, mali ya Mahundi.

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta...

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as...

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...