Skip to main content

Tiba Bora Ya Mwili Na Afya Yako Ni Hii Hapa

Kuna wakati kama binadamu huwa tunapatwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Yapo magonjwa ambayo huwa tunajua chanzo na tiba yake na mengine huwa hatujui. Kwa kuwa afya ni muhimu sana kwa binadamu, kila mtu hufanya kila linalowezekana kuhakikisha mwili wake uko salama kiafya.

Katika kuhakikisha hili linatimia wapo ambao hutumia dawa za kila aina na wapo pia wengine ambao huamua kutumia tiba mbadala. Yote haya hufanyika ili kupata tiba bora ya mwili na afya zetu. Katika makala hii ya leo tutaangalia tiba nyingine bora ya mwili ambayo haifahamiki na wengi. Tunasema ni bora kwa sababu inatibu magonjwa mengi. Tiba hii ni tiba ya zabibu.

Ikumbukwe Zabibu hulimwa sehemu nyingi sana duniani. Matunda ya zabibu ni matamu sana kwa maana ya ladha nzuri mdomoni. Zabibu ziko za kijani, nyeusi na urujuani(Violet). Pia ziko katika maumbile na ‘saizi’ mbalimbali. Kuna zile zenye maumbile madogo na zina mbegu ndogo na nyingi.

Zabibu ni nzuri sana kwa matatizo ya koo, nywele, ngozi na matatizo ya macho. Vilevile zabibu inaleta hamu ya kula. Zabibu zinasaidia kuondoa kiu, homa, pumu, ukoma, kifua kikuu, matatizo ya sauti na kutapika. Inapunguza gesi tumboni.

Zabibu zinaharibika upesi baada ya kuiva hivyo zinataka matunzo mazuri kwa kuwekwa jokofu au penye baridi baada ya kuvuna. Ili zabibi ifanye kazi, huna budi kuzila nyingi kwa siku. Zabibu hufanya mtu aonekane kijana kwa muda mwingi. Glucose iliyo kwenye zabibu huyeyuka kwa haraka sana mwilini.

Zabibu zinasaidia kwenye mambo mengi sana kama unywaji pombe kupita kiasi yaani ‘Alcoholism’. Matatizo ya unywaji pombe mara kwa mara au kupita kiasi unaweza kuachwa au kupunguzwa kwa kula zabibu kila siku. Zabibu zenyewe zinatoa pombe mwilini.

Harufu ya zabibu inaleta ahueni kwenye kwenye matatizo ya pumu na matatizo ya watoto wadogo. Juisi ya zabibu inasaidia kutibu matatizo ya choo kwa watoto wadogo, hata kwa wakubwa inasaidia. Zabibu inasaidia kupunguza matatizo ya moyo na matatizo ya figo.

Zabibu pia inasaidia matatizo ya ini kwa sababu ina tindikali aina ya Malic, Citric na Tartaric. Tindikali hizi zinasaidia kusafisha damu, kuamsha ufanyaji kazi wa tumbo na ini.

Hayo ndiyo magonjwa yanayoweza kutibiwa kwa kutumia Zabibu. Hivyo, ni muhimu sana kwa miili yetu.

Tunakutakia siku njema na afya bora, ila kama umesoma makala hii mshirikishe na mwingine ili apate tiba hii bora bila kuikosa.
                                            @muungwana.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyin