Skip to main content

Mambo matano ya kufahamu kabla ya KRC Genk ya Samatta kucheza vs Celta Vigo leo

Rama Mwelondo TZA

  Usiku wa leo April 13 2017 mtanzaniaMbwana Samatta ataandika historia mpya katika maisha yake ya soka kwa kucheza game yake ya kwanza ya robo fainali ya UEFA Europa League akiwa na KRC Genk kwa mara ya kwanza katika maisha yake.


Mbwana Samatta
KRC Genk wanacheza dhidi ya Celta Vigo leo saa 22:05 kwa saa za Afrika Mashariki, Genk ya Samatta itakuwaHispania kucheza dhidi ya Celta Vigokatika game hiyo ya robo fainali itakayochezwa katika uwanja wa Balaidos, kuelekea game hiyo mtu wangu naomba nikupe dondoo muhimu za Celta vsGenk.

Ratiba ya mechi za robo fainali ya kwanza ya UEFA Europa League zinazochezwa usiku wa leo April 13 2017.
  • Mbwana Samatta anatajwa kama mchezaji wa kuchungwa katika game hiyo, kutokana na takwimu zake za kucheza mechi 6 za Genk zilizopita za mashindano yote na kufunga magoli sita ni wastani wa kufunga goli moja kila mechi.
  • KRC Genk wanaingia kucheza mchezo dhidi ya Celta Vigo wakiwa wanarekodi ya kucheza mechi zao sita za hivi karibuni na kutoruhusu kupoteza mchezo wowote, katika mechi sita Genk wameshinda mechi 5 na kutoa sare mechi moja.
  • Katika mechi tano zilizopita za mashindano yote KRC Genk wamefanikiwa kushinda mechi nne na kutoka sare mechi moja wakati Celta Vigo wameshinda mechi zao tatu na kufungwa mechi mbili.
  • Katika mechi 5 za karibuni Celta Vigo wamefunga jumla ya magoli 8 na kuruhusu magoli 6 wakati KRC Genk wao wamefunga jumla ya magoli 15 na kuruhusu kufungwa magoli matatu.
  • Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa KRC Genk kucheza dhidi ya Celta Vigo katika mashindano yanayoandaliwa na UEFA.
  • Samatta hadi sasa amecheza jumla ya game kumi za UEFA Europa League kuanzia hatua ya makundi, akifunga magoli mawili na kutoa assist moja na hajaoneshwa kadi yoyote ile.
                                    Tembelea millardayo.com

Comments

Popular posts from this blog

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...

Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi

Hii Ndiyo Tafsiri sahihi Ya Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi Moja ya kitu ambacho huwa hakina kipaumbele sana katika mahusiano ya kimapenzi,  kitu ambacho kinachoitwa zawadi. Lakini ukweli ni kwamba zawadi ina maana kubwa sana katika mahusiano ya kimapenzi zaidi hata udhaniavyo. Na Katika tafiti ambazo zimewahi fanywa ni kwamba, suala zima la utoaji zawadi katika mahusiano ya kimapenzi lilimekuwa likileta hisia zaidi katika upande mmoja. Yaani hapa nikiwa na maana ya kwamba jinsia ya kike ndiyo ambayo ipo katika kusubiri zawadi kutoka kwa jinsia ya kiume. Kutoka na suala hilo ndo maana watu wengi wamekuwa hawatilii maanani suala zima la zawadi. Lakini ukweli ni kwamba kila mtu anahusika kutoa zawadi. Huenda ukawa bado nakuacha njia panda huelewi ni zawadi gani ambayo itampendeza mpenzi wako. Wala usipate tabu afisa Mipango nipo kwa ajili yako. Ipo hivi ili kujua zawadi ambayo mwezi wako anapendezwa nayo,  Unachotakiwa kukifanya ni kwamba kwa kuwa ni mpen...