Skip to main content

Mambo matano ya kufahamu kabla ya KRC Genk ya Samatta kucheza vs Celta Vigo leo

Rama Mwelondo TZA

  Usiku wa leo April 13 2017 mtanzaniaMbwana Samatta ataandika historia mpya katika maisha yake ya soka kwa kucheza game yake ya kwanza ya robo fainali ya UEFA Europa League akiwa na KRC Genk kwa mara ya kwanza katika maisha yake.


Mbwana Samatta
KRC Genk wanacheza dhidi ya Celta Vigo leo saa 22:05 kwa saa za Afrika Mashariki, Genk ya Samatta itakuwaHispania kucheza dhidi ya Celta Vigokatika game hiyo ya robo fainali itakayochezwa katika uwanja wa Balaidos, kuelekea game hiyo mtu wangu naomba nikupe dondoo muhimu za Celta vsGenk.

Ratiba ya mechi za robo fainali ya kwanza ya UEFA Europa League zinazochezwa usiku wa leo April 13 2017.
  • Mbwana Samatta anatajwa kama mchezaji wa kuchungwa katika game hiyo, kutokana na takwimu zake za kucheza mechi 6 za Genk zilizopita za mashindano yote na kufunga magoli sita ni wastani wa kufunga goli moja kila mechi.
  • KRC Genk wanaingia kucheza mchezo dhidi ya Celta Vigo wakiwa wanarekodi ya kucheza mechi zao sita za hivi karibuni na kutoruhusu kupoteza mchezo wowote, katika mechi sita Genk wameshinda mechi 5 na kutoa sare mechi moja.
  • Katika mechi tano zilizopita za mashindano yote KRC Genk wamefanikiwa kushinda mechi nne na kutoka sare mechi moja wakati Celta Vigo wameshinda mechi zao tatu na kufungwa mechi mbili.
  • Katika mechi 5 za karibuni Celta Vigo wamefunga jumla ya magoli 8 na kuruhusu magoli 6 wakati KRC Genk wao wamefunga jumla ya magoli 15 na kuruhusu kufungwa magoli matatu.
  • Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa KRC Genk kucheza dhidi ya Celta Vigo katika mashindano yanayoandaliwa na UEFA.
  • Samatta hadi sasa amecheza jumla ya game kumi za UEFA Europa League kuanzia hatua ya makundi, akifunga magoli mawili na kutoa assist moja na hajaoneshwa kadi yoyote ile.
                                    Tembelea millardayo.com

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyin