Skip to main content

VITU VITANO AMBAVYO MATAJIRI WAMEJIFUNZA NA KUVISHIKA KATIKA MAISHA YAO


Kama wewe ni mjasiriamali au unapenda ujasiriamali basi moja kati ya malengo yako ni kufikia utajiri. Hamu hii ya kufikia utajiri inatufanya tupige kazi usiku na mchana bila kuchoka. Tunapowaona wale waliotajirika tayari tunatamani kujua siri zao za mafanikio ili na sisi tuweze kuwa kama wao au zaidi. Mimi binafsi nimekuwa na hamu kubwa ya kujua siri hizi toka nina miaka 12. Ni muda huo ambapo nilianza kusoma vitabu mbalimbali vya wafanyabiashara na kufuatilia maisha yao kiujumla. Toka muda huo na hadi sasa nikiwa nimetimiza miaka 21 nimegundua kuwa kuna vitu vitano vikuu ambavyo wajasiriamali matajiri huwa navyo ambavyo vimewawezesha kufikia hapo walipo.

1. USHAWISHI
Ujasiriamali sio spotispoti. Masaa mengi ya kazi, hatari ya kutofanikiwa na misukosuko ni kawaida. Kuamua kujikita katika jambo hili ni kati ya maamuzi magumu mtu unaweza kufanya. Hii ni kwa sababu kama una familia basi muda na familia yako utapungua sana. Kama wewe ni mtu wa marafiki na viwanja basi itabidi upunguze. Na zaidi ya hapo mara nyingine wakati unaanza biashara au wakati tayari umeshaanza utahitaji kushawishi watu wakufanyie mambo mbalimbali. Umshawishi mtu anunue bidhaa yako, umshawishi ofisa wa benki akupe mkopo au umshawishi rafiki yako aungane nawe katika biashara yako. Ni ushawishi kila sehemu. Bila ushawishi huwezi kusogea mbele katika ujasiriamali.

2. JINSI YA KUAJIRI WATU WANAOFAA
Ni rahisi sana biashara kusambaratika kwa sababu ya wafanyakazi wabovu. Juzi kati moja ya watu ninaowafahamu ilibidi amfukuze msimamizi wake wa saluni kwa sababu hakuwa mwaminifu katika mauzo ya saluni. Kuna uwezekano mkubwa wewe pia ukawa umesikia stori kama hizi mtaani. Hebu sasa fikiria kama mtu kama Mengi angekuwa na watu kama hawa katika kampuni yake ingewezekana kufika hapo alipo leo? Jinsi ya kutambua mfanyakazi bora ni kati ya sehemu muhimu sana katika kukuza biashara. Wafanyakazi wazuri watakuza mauzo yako. Wafanyakazi wazuri watakufanya uwe tajiri. Lenga kujenga uwezo huu na utafika mbali sana katika safari hii ya ujasiriamali.

3. JINSI YA KUTUMIA MUDA WAO VIZURI
Katika siku moja kuna masaa 24. Hakuna siku utaongezewa hata sekunde moja. Na yakipita hayarudi tena. Kama mjasiriamali huwa najiuliza swali moja ninapoamka. Leo nitafanya nini kuboresha biashara yangu? Vitu vingine ambavyo najiuliza mara kwa mara ni nimepoteza muda wapi leo? Nifanye nini ili kitu hiki kichukue muda mfupi zaidi kumaliza? Nimpe nani kazi hii ili muda huu niutumie kufanya kitu muhimu zaidi? Ni maswali haya ambayo yananipelekea kuepuka kuingia Youtube kwa sababu huwa naishia kutumia muda mwingi humo halafu sifanyi cha maana. Ni maswali haya ambayo yananipelekea kutafuta mbinu za kufanya vitu haraka zaidi kila siku. Ni maswali haya ambayo yananipelekea nilipe watu wafanye kazi mbalimbali ili niwe huru kufanya mambo ya muhimu kama kuandika makala hii. Hebu kaa ufikirie je leo umetumia muda wako vizuri? Kumbuka, kushinda instagram ukifuatilia vita ya yule dada wa Marekani na serikali hakutazogeza biashara yako mbele. Kama hutaki kabisa kupitwa na ubuyu tenga dakika tano kwa siku kuchungulia inatosha…

4. MATUMIZI MAZURI YA PESA
Ukichunguza matajiri wajasiriamali utaona kuwa wanaheshimu utajiri wao. Wanajua kuwa kupata pesa tu haitoshi inabidi uweze kuitunza pesa vizuri na kisha uitumie hiyo pesa uliyoitunza kupata pesa nyingi zaidi. Utaona watu hawa ambao wengi wameanza wakiwa na mitaji midogo au bila kitu kabisa wakikuza mitaji yao taratibu na hadi wanafikia utajiri mkubwa hawana matumizi ya ovyo ya pesa. Mengi, Bakhresa, Dewji, Rostam Aziz ni kati ya wajasiriamali wakubwa nchini. Kwa pesa walizonazo wanaweza kubadilisha magari ya kifahari kila wiki kwa mwaka mzima. Wanaweza kumiliki nyumba za kifahari katika kila mkoa. Wanaweza kununua Iphone 7 za kutosha wakawa wanabadilisha kila siku. Ila hakuna anayefanya hivyo. Japokuwa tayari ni matajiri bado sehemu kubwa ya kipato chao kinaenda katika kukuza biashara zao. Wanaheshimu pesa. Kama mjasiriamali tambua kuwa biashara yako ndio maisha yako. Tumbua pesa zako na biashara yako itakufa. Rudisha kipato katika biashara na utatajirika kupita mategemeo yako

5. KUWA NA FUJO TULIVU
Wote tunamjua angalau mtu mmoja ambaye ana fujo sana. Huyu ni yule rafiki yako ambaye ugomvi ukitokea aidha kauanzisha au yupo mstari wa mbele kwenye mapigano. Huyu ni yule mbishi ambaye hakubali kushindwa. Yakitokea mabishano tu basi ukiwa upande wake ushashinda. Katika ujasiriamali unahitaji kuwa na fujo. Ila hapa nimeongelea fujo tulivu. Namaanisha nini? Utakutana na misukosuko katika biashara. Mtu mwenye fujo tulivu atapigika, kisha atanyanyuka na kuendelea kusonga mbele bila kulalamika. Safari kuelekea utajiri itachukua muda mrefu kuliko unavyodhania. Mtu mwenye fujo tulivu hatakata tamaa na kuishia njiani, ataendelea kupiga kazi mpaka kieleweke. Kuna kipindi washindani watataka kukuchukulia wateja wako. Mtu mwenye fujo tulivu hataenda kuanzisha timbwili katika ofisi za washindani wake, bali atapigana kuboresha huduma zake ili abakize wateja wake na aongeze wengi zaidi. Kichwani mwa mtu mwenye fujo tulivu tayari yeye ashakuwa tajiri. Hajali changamoto, hajali misukosuko, hajali chochote. Yeye kashaweka lengo la kufikia utajiri na hakuna kitu duniani au kwingineko kitamzuia kufikia lengo lake.  Kichwani mwake hadi Mungu tayari yupo katika upande wake hivyo hawezi kushindwa.

Hivyo ndivyo vitu vitano vikuu ambavyo matajiri wajasiriamali wanavyo. Kama wewe pia unataka kuwa tajiri basi hii ni fursa kwako ya kuanza kujifunza vitu hivi vikuu ili uweze kusogea karibu zaidi na lengo lako ya kuwa tajiri.

Comments

Popular posts from this blog

je wajua,zifahamu mbinu mbalimbali za kumpata mwenzi bora

KILA mtu anapenda kuwa na mwenza mzuri, mwenye kumfaa katika maisha yake. Hata hivyo kwa bahati mbaya ni kwamba wengi wanashindwa kupata wenza wazuri. Ziko sababu nyingi lakini kubwa ni uwezo wa mtu wa kumtambua mwingine na kujua kama ni kweli anafaa au anafaa  kuendana nae au la.Wakati wa uchumba, wengi wa watu huonekana kutumiana kadi, zawadi na mambo mengine  mbalimbali yenye lengo la kuonyesha wanapendana. Aidha, wapo ambao wanashindwa kujua namna ya kutongoza; kwa ujumla kutongoza ni uwezo wa ushawishi kwamba unamwambia mwanamke unamuhitaji na kumpenda awe wako au wakati mwingine hata mwanamke anaweza kuanza. Ndio ukweli wenyewe Sio kweli kwamba kila mwanaume anajua kutongoza. Kuna wengine hata kumsimamisha mwanamke hawezi au anaogopa. Ndio unaweza kukuta mwanamume anajikanyaga namna ya kuongea. Wapo wengine wanafikiri njia sahihi ya kutongoza ni kuhonga aidha fedha au mali nk, lakini sicho hasa wanachotaka wanawake au wanaume katika mapenzi. Maneno ya ku...

Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi

Hii Ndiyo Tafsiri sahihi Ya Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi Moja ya kitu ambacho huwa hakina kipaumbele sana katika mahusiano ya kimapenzi,  kitu ambacho kinachoitwa zawadi. Lakini ukweli ni kwamba zawadi ina maana kubwa sana katika mahusiano ya kimapenzi zaidi hata udhaniavyo. Na Katika tafiti ambazo zimewahi fanywa ni kwamba, suala zima la utoaji zawadi katika mahusiano ya kimapenzi lilimekuwa likileta hisia zaidi katika upande mmoja. Yaani hapa nikiwa na maana ya kwamba jinsia ya kike ndiyo ambayo ipo katika kusubiri zawadi kutoka kwa jinsia ya kiume. Kutoka na suala hilo ndo maana watu wengi wamekuwa hawatilii maanani suala zima la zawadi. Lakini ukweli ni kwamba kila mtu anahusika kutoa zawadi. Huenda ukawa bado nakuacha njia panda huelewi ni zawadi gani ambayo itampendeza mpenzi wako. Wala usipate tabu afisa Mipango nipo kwa ajili yako. Ipo hivi ili kujua zawadi ambayo mwezi wako anapendezwa nayo,  Unachotakiwa kukifanya ni kwamba kwa kuwa ni mpen...

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...