Skip to main content

KILIMO CHA TANGAWIZI


Image result for kilimo cha tangawiziImage result for kilimo cha tangawizi


Tangawizi ni moja kati ya mazao ya viungo ambayo sehemu inayotumiwa na binadamu ni tunguu(rhzomes).

     MAZINGIRA YA UMEAJI WA TANGAWIZI
  • Tangawizi huota vizuri katika maeneo ya kitropikali yenye mwinuko kati ya 1200m-1800m kutoka usawa wa bahari.
  • Joto la wastani wa nyuzi 20c-24c huota vizuri.
  • Hustawi vyema katika udongo wenye tifutifu na usiotuamisha maji.
AINA
Mpaka sasa hakuna aina maalumu zilizoainishwa za tangawizi isipokuwa kwa Tanzania zipo aina tatu wanazolima wakulima wetu ambazo ni Cochin,Bombay na White Africa maarufu kama tangawizi nyeupe.

Tangawizi inayopandwa sehemu za milimani huwa ngumu na nyuzinyuzi nyngi (fibre) kuliko zile za maeneo ya tambarare ambazo huwa laini.

NAFASI
Nafasi inayotumika kupandia ni sentimeta 23-30 na 15-23 na kina cha sentimeta 5-10 hutumika.Nafazi za upandaji zinatoautiana kulingana na aina ya udongo,mazingira na aina ya tangawizi inayopandwa.Inashauriwa umwagiliaji wa maji mara kwa mara endapo mvua zinakosekana ili kuruhusu umeaji kwa urahisi.

 MBEGU NA NAMNA YA KUPANDA TANGAWIZI

Kumbuka; Ondoa takataka zote shambani na weka shamba mbolea ya samadi tani 25-30 kwa hekta moja wiki mbili kabla ya kupanda.

Tangawizi hupandwa kwa kutumia vipande vya tunguu (rhizomes).Tangawizi huifadhiwa mahali pakavu penye baridi ili machipukizi kuota.Machipukizi hukatwa kwenye urefu wa sentimeta 2-5.5 na kupelekwa kupandwa shambani.

Baada ya kupanda tandaza matandazo juu ili kuzuia mionzi ya jua isiathiri tangawizi kabla ya kumea.

PALIZI
Katika kipindi cha wiki mbili majani huota kwa kasi kutokana na hali ya unyevunyevu wa udongo hivyo ni nyema kuanza palizi maramoja.

MAGONJWA NA WADUDU

  • MADOADOA KWENYE MAJANI
Ugonjwa wa fangasi unaosababishwa na vimelea viitwavyo Cholectotricum ziberis 
Tumia dawa yoyote ya kuteketeza fangasi wa ardhini ikiwemo BLUE COPPER au RIDOMIL GOLD

  • KUOZA KWA TUNGUU NA MIZIZI FUNDO
Yote ni magonjwa yanayosababishwa na fangasi wa ardhini.
   
       NAMNA YA KUZUIA;
  1. Nyunyizia dawa ya ridomil golg wakati wa kupanda kwa kuchovya mbegu za tangawizi kwenye chombo chenye dawa kuzuia mashambulizi ya fangasi wa ardhini
  2. Wakati wa kusafisha shamba choma majani yote shambani ili kuua wadudu.

Image result for kilimo cha tangawiziUVUNAJI
Tangawizi huweza kuvunwa kwa kipindi cha miezi 8-10 mara tu majani yanapogeuka rangi na kuwa ya njano na mashina kusinyaa.

 Mavuno ya kati ya tani 20-30 kwa hekta moja yanaweza kupatikana hii ni kutokana na huduma mbalimbali zikiwemo  palizi,maji na uwekaji wa mbolea kwa wakati.

MATUMIZI YA TANGAWIZI
Tangawizi hutumika kama kiungo katika vinywaji mbalimbali kama vile chai,soda,juisi na vilevi.Pia hutumika kama kiungo kwa aina mbalimbali za vyakula kama vile biskuti,mikate na achari.

 Pia viwandani tangawizi hutumika kutengenezea dawa mbalimbali za kkikohozi,muasho wa ngozi na zinginezo.Tangawizi hutumika kutengenezea vipodozi kama poda.

SOKO LA TANGAWIZI
Tangawizi inauzika kwa wingi ndani ya nchi na kiasi huuzwa nchi jirani kama vile Kenya na Uganda.
Huuzwa kwa kiasi cha sh.300-2000/= kulingana na msimu wa soko.
            Imechapishwa na 

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyin