Skip to main content

KILIMO CHA TANGAWIZI


Image result for kilimo cha tangawiziImage result for kilimo cha tangawizi


Tangawizi ni moja kati ya mazao ya viungo ambayo sehemu inayotumiwa na binadamu ni tunguu(rhzomes).

     MAZINGIRA YA UMEAJI WA TANGAWIZI
  • Tangawizi huota vizuri katika maeneo ya kitropikali yenye mwinuko kati ya 1200m-1800m kutoka usawa wa bahari.
  • Joto la wastani wa nyuzi 20c-24c huota vizuri.
  • Hustawi vyema katika udongo wenye tifutifu na usiotuamisha maji.
AINA
Mpaka sasa hakuna aina maalumu zilizoainishwa za tangawizi isipokuwa kwa Tanzania zipo aina tatu wanazolima wakulima wetu ambazo ni Cochin,Bombay na White Africa maarufu kama tangawizi nyeupe.

Tangawizi inayopandwa sehemu za milimani huwa ngumu na nyuzinyuzi nyngi (fibre) kuliko zile za maeneo ya tambarare ambazo huwa laini.

NAFASI
Nafasi inayotumika kupandia ni sentimeta 23-30 na 15-23 na kina cha sentimeta 5-10 hutumika.Nafazi za upandaji zinatoautiana kulingana na aina ya udongo,mazingira na aina ya tangawizi inayopandwa.Inashauriwa umwagiliaji wa maji mara kwa mara endapo mvua zinakosekana ili kuruhusu umeaji kwa urahisi.

 MBEGU NA NAMNA YA KUPANDA TANGAWIZI

Kumbuka; Ondoa takataka zote shambani na weka shamba mbolea ya samadi tani 25-30 kwa hekta moja wiki mbili kabla ya kupanda.

Tangawizi hupandwa kwa kutumia vipande vya tunguu (rhizomes).Tangawizi huifadhiwa mahali pakavu penye baridi ili machipukizi kuota.Machipukizi hukatwa kwenye urefu wa sentimeta 2-5.5 na kupelekwa kupandwa shambani.

Baada ya kupanda tandaza matandazo juu ili kuzuia mionzi ya jua isiathiri tangawizi kabla ya kumea.

PALIZI
Katika kipindi cha wiki mbili majani huota kwa kasi kutokana na hali ya unyevunyevu wa udongo hivyo ni nyema kuanza palizi maramoja.

MAGONJWA NA WADUDU

  • MADOADOA KWENYE MAJANI
Ugonjwa wa fangasi unaosababishwa na vimelea viitwavyo Cholectotricum ziberis 
Tumia dawa yoyote ya kuteketeza fangasi wa ardhini ikiwemo BLUE COPPER au RIDOMIL GOLD

  • KUOZA KWA TUNGUU NA MIZIZI FUNDO
Yote ni magonjwa yanayosababishwa na fangasi wa ardhini.
   
       NAMNA YA KUZUIA;
  1. Nyunyizia dawa ya ridomil golg wakati wa kupanda kwa kuchovya mbegu za tangawizi kwenye chombo chenye dawa kuzuia mashambulizi ya fangasi wa ardhini
  2. Wakati wa kusafisha shamba choma majani yote shambani ili kuua wadudu.

Image result for kilimo cha tangawiziUVUNAJI
Tangawizi huweza kuvunwa kwa kipindi cha miezi 8-10 mara tu majani yanapogeuka rangi na kuwa ya njano na mashina kusinyaa.

 Mavuno ya kati ya tani 20-30 kwa hekta moja yanaweza kupatikana hii ni kutokana na huduma mbalimbali zikiwemo  palizi,maji na uwekaji wa mbolea kwa wakati.

MATUMIZI YA TANGAWIZI
Tangawizi hutumika kama kiungo katika vinywaji mbalimbali kama vile chai,soda,juisi na vilevi.Pia hutumika kama kiungo kwa aina mbalimbali za vyakula kama vile biskuti,mikate na achari.

 Pia viwandani tangawizi hutumika kutengenezea dawa mbalimbali za kkikohozi,muasho wa ngozi na zinginezo.Tangawizi hutumika kutengenezea vipodozi kama poda.

SOKO LA TANGAWIZI
Tangawizi inauzika kwa wingi ndani ya nchi na kiasi huuzwa nchi jirani kama vile Kenya na Uganda.
Huuzwa kwa kiasi cha sh.300-2000/= kulingana na msimu wa soko.
            Imechapishwa na 

Comments

Popular posts from this blog

je wajua,zifahamu mbinu mbalimbali za kumpata mwenzi bora

KILA mtu anapenda kuwa na mwenza mzuri, mwenye kumfaa katika maisha yake. Hata hivyo kwa bahati mbaya ni kwamba wengi wanashindwa kupata wenza wazuri. Ziko sababu nyingi lakini kubwa ni uwezo wa mtu wa kumtambua mwingine na kujua kama ni kweli anafaa au anafaa  kuendana nae au la.Wakati wa uchumba, wengi wa watu huonekana kutumiana kadi, zawadi na mambo mengine  mbalimbali yenye lengo la kuonyesha wanapendana. Aidha, wapo ambao wanashindwa kujua namna ya kutongoza; kwa ujumla kutongoza ni uwezo wa ushawishi kwamba unamwambia mwanamke unamuhitaji na kumpenda awe wako au wakati mwingine hata mwanamke anaweza kuanza. Ndio ukweli wenyewe Sio kweli kwamba kila mwanaume anajua kutongoza. Kuna wengine hata kumsimamisha mwanamke hawezi au anaogopa. Ndio unaweza kukuta mwanamume anajikanyaga namna ya kuongea. Wapo wengine wanafikiri njia sahihi ya kutongoza ni kuhonga aidha fedha au mali nk, lakini sicho hasa wanachotaka wanawake au wanaume katika mapenzi. Maneno ya ku...

Aliyoyajibu Lulu Diva baada ya kudaiwa kuwa mapenzini na Madee

Aliyoyajibu Lulu Diva baada ya kudaiwa kuwa mapenzini na Madee April 6, 2017 kupitia U heard ya XXL ya Clouds FM staa wa Bongo Fleva Lulu Diva ameweka wazi uhusiano wake na staa mwingine wa Bongo Fleva kutoka Tip Top Connection,   Madee baada ya kuonekana mara kwa mara wakiwa pamoja. Soudy Brown aliwatafuta Madee na Lulu Diva kufahamu ukweli ambapo Madee hakupatikana kwenye simu, lakini Lulu Diva alikuwa na haya ya kujibu alipoulizwa kuhusu kutoka kimapenzi na Madee . ..>>> “Madee ni kaka yangu na nimshauri wangu halafu pia kuna wimbo wake amenishirikisha, Soudy na wewe umezidi umbea, T-shirt akivaa Madee sisi wengine hatuwezi kununua? T-shirt tumenunua sare, tumenunua siku moja.”  – Lulu Diva.

Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi

Hii Ndiyo Tafsiri sahihi Ya Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi Moja ya kitu ambacho huwa hakina kipaumbele sana katika mahusiano ya kimapenzi,  kitu ambacho kinachoitwa zawadi. Lakini ukweli ni kwamba zawadi ina maana kubwa sana katika mahusiano ya kimapenzi zaidi hata udhaniavyo. Na Katika tafiti ambazo zimewahi fanywa ni kwamba, suala zima la utoaji zawadi katika mahusiano ya kimapenzi lilimekuwa likileta hisia zaidi katika upande mmoja. Yaani hapa nikiwa na maana ya kwamba jinsia ya kike ndiyo ambayo ipo katika kusubiri zawadi kutoka kwa jinsia ya kiume. Kutoka na suala hilo ndo maana watu wengi wamekuwa hawatilii maanani suala zima la zawadi. Lakini ukweli ni kwamba kila mtu anahusika kutoa zawadi. Huenda ukawa bado nakuacha njia panda huelewi ni zawadi gani ambayo itampendeza mpenzi wako. Wala usipate tabu afisa Mipango nipo kwa ajili yako. Ipo hivi ili kujua zawadi ambayo mwezi wako anapendezwa nayo,  Unachotakiwa kukifanya ni kwamba kwa kuwa ni mpen...