Skip to main content

KILIMO CHA TANGAWIZI


Image result for kilimo cha tangawiziImage result for kilimo cha tangawizi


Tangawizi ni moja kati ya mazao ya viungo ambayo sehemu inayotumiwa na binadamu ni tunguu(rhzomes).

     MAZINGIRA YA UMEAJI WA TANGAWIZI
  • Tangawizi huota vizuri katika maeneo ya kitropikali yenye mwinuko kati ya 1200m-1800m kutoka usawa wa bahari.
  • Joto la wastani wa nyuzi 20c-24c huota vizuri.
  • Hustawi vyema katika udongo wenye tifutifu na usiotuamisha maji.
AINA
Mpaka sasa hakuna aina maalumu zilizoainishwa za tangawizi isipokuwa kwa Tanzania zipo aina tatu wanazolima wakulima wetu ambazo ni Cochin,Bombay na White Africa maarufu kama tangawizi nyeupe.

Tangawizi inayopandwa sehemu za milimani huwa ngumu na nyuzinyuzi nyngi (fibre) kuliko zile za maeneo ya tambarare ambazo huwa laini.

NAFASI
Nafasi inayotumika kupandia ni sentimeta 23-30 na 15-23 na kina cha sentimeta 5-10 hutumika.Nafazi za upandaji zinatoautiana kulingana na aina ya udongo,mazingira na aina ya tangawizi inayopandwa.Inashauriwa umwagiliaji wa maji mara kwa mara endapo mvua zinakosekana ili kuruhusu umeaji kwa urahisi.

 MBEGU NA NAMNA YA KUPANDA TANGAWIZI

Kumbuka; Ondoa takataka zote shambani na weka shamba mbolea ya samadi tani 25-30 kwa hekta moja wiki mbili kabla ya kupanda.

Tangawizi hupandwa kwa kutumia vipande vya tunguu (rhizomes).Tangawizi huifadhiwa mahali pakavu penye baridi ili machipukizi kuota.Machipukizi hukatwa kwenye urefu wa sentimeta 2-5.5 na kupelekwa kupandwa shambani.

Baada ya kupanda tandaza matandazo juu ili kuzuia mionzi ya jua isiathiri tangawizi kabla ya kumea.

PALIZI
Katika kipindi cha wiki mbili majani huota kwa kasi kutokana na hali ya unyevunyevu wa udongo hivyo ni nyema kuanza palizi maramoja.

MAGONJWA NA WADUDU

  • MADOADOA KWENYE MAJANI
Ugonjwa wa fangasi unaosababishwa na vimelea viitwavyo Cholectotricum ziberis 
Tumia dawa yoyote ya kuteketeza fangasi wa ardhini ikiwemo BLUE COPPER au RIDOMIL GOLD

  • KUOZA KWA TUNGUU NA MIZIZI FUNDO
Yote ni magonjwa yanayosababishwa na fangasi wa ardhini.
   
       NAMNA YA KUZUIA;
  1. Nyunyizia dawa ya ridomil golg wakati wa kupanda kwa kuchovya mbegu za tangawizi kwenye chombo chenye dawa kuzuia mashambulizi ya fangasi wa ardhini
  2. Wakati wa kusafisha shamba choma majani yote shambani ili kuua wadudu.

Image result for kilimo cha tangawiziUVUNAJI
Tangawizi huweza kuvunwa kwa kipindi cha miezi 8-10 mara tu majani yanapogeuka rangi na kuwa ya njano na mashina kusinyaa.

 Mavuno ya kati ya tani 20-30 kwa hekta moja yanaweza kupatikana hii ni kutokana na huduma mbalimbali zikiwemo  palizi,maji na uwekaji wa mbolea kwa wakati.

MATUMIZI YA TANGAWIZI
Tangawizi hutumika kama kiungo katika vinywaji mbalimbali kama vile chai,soda,juisi na vilevi.Pia hutumika kama kiungo kwa aina mbalimbali za vyakula kama vile biskuti,mikate na achari.

 Pia viwandani tangawizi hutumika kutengenezea dawa mbalimbali za kkikohozi,muasho wa ngozi na zinginezo.Tangawizi hutumika kutengenezea vipodozi kama poda.

SOKO LA TANGAWIZI
Tangawizi inauzika kwa wingi ndani ya nchi na kiasi huuzwa nchi jirani kama vile Kenya na Uganda.
Huuzwa kwa kiasi cha sh.300-2000/= kulingana na msimu wa soko.
            Imechapishwa na 

Comments

Popular posts from this blog

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...

KILIMO CHA KISASA CHA MPUNGA

Utangulizi Mpunga ni zao la pili la chakula kwa umuhimu linalolimwa sehemu nyingi nchini Tanzania. Umuhimu wa zao hili umeongezeka kuanzia muongo uliopita kutokana na jamii za mijini na vijijini kupendelea zaidi kula wali na kupunguza ulaji wa vyakula vingine na kulifanya zao hili kuwa la chakula na biashara. Mvua ni chanzo kikuu cha maji kwenye kilimo cha mpunga. Viwango vya mahitaji ya maji katika kukua kwa mpunga hutofautiana miongoni mwa aina za mpunga. Ni kwa jinsi hii mpunga hupandwa katika mazingira mbalimbali kutegemea na mahitaji yake ya maji. Zipo aina tatu kuu za mazingira yanayolimwa mpunga kulingana na upatikanaji wa maji na hali ya mwinuko wa nchi. Mazingira haya ni kilimo cha mpunga wa mabondeni kinachotegemea mvua (72%), kilimo cha mpunga wa kwenye miinuko (20%) na kilimo cha mpunga cha umwagiliaji (8%). Kiasi cha mpunga kinachozalishwa nchini kimekuwa kikiongezeka mwaka hadi mwaka kutoka tani 41,000 mwaka 1970 hadi tani 811,500 mwaka 1998. Ongezeko hi...