Skip to main content

Hakuna njaa, kuna uhaba wa fedha -Tizeba

WAZIRI wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Charles Tizeba amebainisha kuwa kwa sasa Tanzania hakuna tatizo la njaa kutokana na masoko mengi kuwa na chakula isipokuwa tatizo lililopo ni uhaba wa fedha.

Waziri Tizeba aliyasema hayo alipokutana na baadhi ya wananchi kwenye maeneo ya soko kuu mjini Shinyanga alipopita akienda mkoani Dodoma kuendelea kushiriki katika vikao vya Bunge la bajeti vinavyoendelea mkoani humo.

Tizeba alitolea ufafanuzi suala la madai ya kuwepo kwa njaa katika baadhi ya maeneo hapa nchini na kufafanua kuwa kinachodaiwa ni njaa ni uhaba wa fedha kwa baadhi ya watu kwa vile tafiti zilizofanywa na serikali katika maeneo mengi zimeonesha uwepo wa chakula katika masoko mengi.

“Wananchi wenzangu si kweli hapa nchini tuna janga la njaa, nasema kwa ushahidi ninyi wenyewe tembeleeni maeneo mbalimbali katika masoko yetu mtajionea hali halisi, vyakula ni vingi tatizo ni uhaba wa fedha kwa baadhi ya watu, sasa hii huwezi kusema ni njaa,” alisema.

Alisema wapo baadhi ya wanasiasa wanaishinikiza serikali itoe chakula cha akiba ili kigawiwe bure au kiuzwe kwa bei nafuu kwa wananchi, jambo ambalo ni kukurupuka kwani kikiuzwa kwa bei rahisi kitakapomalizika wafanyabiashara watapata mwanya wa kuuza vyakula walivyonavyo kwa bei kubwa.

Kuhusu suala la uwepo wa wadudu waharibifu wa mazao katika maeneo mengi nchini, waziri huyo alisema tatizo hilo linachangiwa na ugumu wa kukabiliana na wadudu hao kutokana na mashamba mengi kulimwa kwenye maeneo ya makazi ya watu.

“Tunawashauri wakulima wetu kwa hili hakuna sababu ya kusubiri serikali, waungane watatu ama watano wanunue vifaa pamoja na dawa za kuulia wadudu hawa, bei si kubwa wanaweza kunyunyuzia kwa kupeana zamu, sisi serikali tutafanya kazi hii kwenye mashamba makubwa,” alisema.

Hata hivyo alikiri kuwepo kwa ongezeko la bei ya sukari katika maeneo mengi nchini kwani kwa mujibu wa taarifa za wiki iliyopita baadhi ya maeneo kilo moja ya sukari ilikuwa ikiuzwa kwa Sh 3,000, hali iliyochangiwa na viwanda kusimamisha uzalishaji kipindi hiki cha masika.

Comments

Popular posts from this blog

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta...