Skip to main content

Hakuna njaa, kuna uhaba wa fedha -Tizeba

WAZIRI wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Charles Tizeba amebainisha kuwa kwa sasa Tanzania hakuna tatizo la njaa kutokana na masoko mengi kuwa na chakula isipokuwa tatizo lililopo ni uhaba wa fedha.

Waziri Tizeba aliyasema hayo alipokutana na baadhi ya wananchi kwenye maeneo ya soko kuu mjini Shinyanga alipopita akienda mkoani Dodoma kuendelea kushiriki katika vikao vya Bunge la bajeti vinavyoendelea mkoani humo.

Tizeba alitolea ufafanuzi suala la madai ya kuwepo kwa njaa katika baadhi ya maeneo hapa nchini na kufafanua kuwa kinachodaiwa ni njaa ni uhaba wa fedha kwa baadhi ya watu kwa vile tafiti zilizofanywa na serikali katika maeneo mengi zimeonesha uwepo wa chakula katika masoko mengi.

“Wananchi wenzangu si kweli hapa nchini tuna janga la njaa, nasema kwa ushahidi ninyi wenyewe tembeleeni maeneo mbalimbali katika masoko yetu mtajionea hali halisi, vyakula ni vingi tatizo ni uhaba wa fedha kwa baadhi ya watu, sasa hii huwezi kusema ni njaa,” alisema.

Alisema wapo baadhi ya wanasiasa wanaishinikiza serikali itoe chakula cha akiba ili kigawiwe bure au kiuzwe kwa bei nafuu kwa wananchi, jambo ambalo ni kukurupuka kwani kikiuzwa kwa bei rahisi kitakapomalizika wafanyabiashara watapata mwanya wa kuuza vyakula walivyonavyo kwa bei kubwa.

Kuhusu suala la uwepo wa wadudu waharibifu wa mazao katika maeneo mengi nchini, waziri huyo alisema tatizo hilo linachangiwa na ugumu wa kukabiliana na wadudu hao kutokana na mashamba mengi kulimwa kwenye maeneo ya makazi ya watu.

“Tunawashauri wakulima wetu kwa hili hakuna sababu ya kusubiri serikali, waungane watatu ama watano wanunue vifaa pamoja na dawa za kuulia wadudu hawa, bei si kubwa wanaweza kunyunyuzia kwa kupeana zamu, sisi serikali tutafanya kazi hii kwenye mashamba makubwa,” alisema.

Hata hivyo alikiri kuwepo kwa ongezeko la bei ya sukari katika maeneo mengi nchini kwani kwa mujibu wa taarifa za wiki iliyopita baadhi ya maeneo kilo moja ya sukari ilikuwa ikiuzwa kwa Sh 3,000, hali iliyochangiwa na viwanda kusimamisha uzalishaji kipindi hiki cha masika.

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyin