Skip to main content

Waafrika wanauzwa Libya katika biashara ya Utumwa

Ripoti ya IOM yasema kuwa wahamiaji wa kiafrika wananunuliwa na kuuzwa katika LibyaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionRipoti ya IOM yasema kuwa wahamiaji wa kiafrika wananunuliwa na kuuzwa katika Libya
Raia wa Afrika wanaojaribu kuvuka na kuelekea barani Ulaya, wanauzwa na watekaji wao na kuuzwa katika "soko la utumwa" nchini Libya. Hayo yamesemwa na shirika la kuwahudumia wahamiaji duniani International Organization for Migration (IOM).
Wahasiriwa wameiambia IOM kuwa, baada ya kuzuiliwa na walanguzi wa biashara ya watu au makundi ya wapiganaji, wanapelekwa hadi kwenye viwanja vya mji au kwenye maeneo ya kuegeshea magari na kuuzwa.
Wahamiaji walio na ujuzi kama vile upakaji rangi au ukulima, wanauzwa kwa bei ya juu, kiongozi mkuu wa shirika hilo la IOM nchini Libya ameiambia BBC
Libya imekuwa katika ghasia tangu mwaka 2011 pale wanajeshi wa shirika la kujihami la mataifa ya magharibi-NATO yalipomuondoa madarakani Rais wa nchi hiyo Kanali Muammar Gaddafi.
IOM yasema matendo ya Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionIOM yasema matendo ya "kutisha" dhidi ya wahamiaji inajumuisha kula chakula kidogo, kuuwawa au kuachwa wafe njaa
Kwa mjibu wa IOM, maelfu ya wanaume chipukizi kutoka mataifa ya kusini mwa jangwa la Sahara wameuzwa katika masoko hayo ya utumwa wa binadamu.
Mhamiaji mmoja kutoka Senegal, ambaye jina lake limebanwa ili kumlinda, amesema kuwa amewahi kuuzwa katika masoko kama hayo katika mji wa Sabha kusini mwa Libya, kabla ya kuwekwa katika gereza moja bovu, ambapo zaidi ya wahamiaji 100 walikuwa wakizuiwa.
Kila mwaka maelfu ya wahamiaji huvuka bahari ya Mediterranean kuelekea Bara UlayaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionKila mwaka maelfu ya wahamiaji huvuka bahari ya Mediterranean kuelekea Bara Ulaya
Amesema kwamba, wahamiaji wanaozuiliwa waliambiwa kuwapigia simu familia zao, ambao waliulizwa kutoa fedha ya kikombozi ili waachiwe huru, na baadhi yao wakapigwa wakiwa bado wanazungumza kwenye simu, ili kuwafanya jamaa zao wasikie wakiteswa ili watume haraka fedha hizo.
Ameelezea kuwa ni matendo ya "kutisha" ambapo wahamiaji walilazimishwa kuhimili kula kiwango kidogo mno cha chakula, lakini kwa wale wasioweza kulipia wanauwawa au wanaachwa ili wafe njaa, ripoti hiyo inaongeza.
Ramani inayoonyesha namna uhamiaji huwa kutoka Bara la Afrika hadi UlayaHaki miliki ya pichaUNICEF
Image captionRamani inayoonyesha namna uhamiaji huwa kutoka Bara la Afrika hadi Ulaya
Mfanyikazi mmoja wa IOM nchini Niger, amesema kwamba ripoti ya biashara ya utumwa nchini Libya ni ya hakika, baada ya kuzungumza na wahamiaji waliotoroka kutoka kambi za kuwazuilia wahamiaji.
"Wote walielezea hatari ya kuuzwa walipokuwa wamezuiliwa kwenye viwanja na karakana za magari huko Sabha, aidha na madereva wao au wenyeji wanaowaandikisha wahamiaji kufanya vibarua vya kila siku mjini humo, wengi wao kama wajenzi.
"Baadaye, badala ya kulipwa, wanauza kwa wanunuzi wapya."
Baadhi ya wahamiaji, wengi wao kutoka Nigeria, Ghana na Gambians wanalazimishwa kufanya kazi" kama walinzi katika majumba ya kupokea fedha za kikombozi au katika 'soko lenyewe", mfanyikazi huyo wa IOM aliongeza. Tembelea BBC.COM

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyin