Skip to main content

Mfumo Matumizi za EFDs wabadilishwa

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imefanya mabadiliko katika mfumo wa usimamizi wa matumizi ya Mashine za kielektroniki za Utoaji risiti (EFDMS) ili kudhibiti uwezekano wa kughushi risiti.
Aidha, mfumo huo una usalama wa hali ya juu, kwani miamala na risiti zote zitakuwa na saini ya kielektroniki na “QR Code”, hivyo kupunguza uwezekano wa kughushi risiti kutoka kwenye mashine za kielektroniki ambazo hazijasajiliwa na mfumo wa mamlaka hiyo.
Akizungumza wakati wa kufungua semina ya Walipakodi Wakubwa, Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA, Neema Mrema alisema mfumo huo ni wa kiintelijensia kwani una uwezo wa kutambua hati ya mauzo kwa mkopo, marejesho ya mauzo, risiti halali na durufu.
“Mfumo umezingatia kupunguza gharama, kwani mfumo huu ni wa Tehama ambao utaipunguzia gharama serikali kununua mashine halisi kwa kuwa umeunganishwa na seva ya TRA,” alisema Neema.
Alisema mfumo huo pia una ufanisi mkubwa na ni rafiki kwani unaweza kuunganishwa na mifumo mingine kama mifumo ya ankara, mauzo na stakabadhi mbalimbali kwa kufanya mabadiliko machache, pia unaruhusu matumizi ya fedha mbalimbali.
Semina hiyo ya siku moja imewakutanisha walipakodi wakubwa kwa ajili ya kupata elimu juu ya Sheria ya fedha ya mwaka 2016 na Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ya mwaka 2014.
Mada zingine zilizowasilishwa ni kodi ya zuio katika bidhaa na huduma, mfumo wa ukusanyaji wa maduhuli kwa kutumia mashine za kielektroniki za utoaji risiti (vitual EFD).
Akizungumzia kodi ya zuio, Neema alisema utekelezaji wa Kodi ya zuio iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2013 umekuwa na changamoto mbalimbali kwa idara na taasisi za serikali.
                                                    Tembelea muungwana.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

je wajua,zifahamu mbinu mbalimbali za kumpata mwenzi bora

KILA mtu anapenda kuwa na mwenza mzuri, mwenye kumfaa katika maisha yake. Hata hivyo kwa bahati mbaya ni kwamba wengi wanashindwa kupata wenza wazuri. Ziko sababu nyingi lakini kubwa ni uwezo wa mtu wa kumtambua mwingine na kujua kama ni kweli anafaa au anafaa  kuendana nae au la.Wakati wa uchumba, wengi wa watu huonekana kutumiana kadi, zawadi na mambo mengine  mbalimbali yenye lengo la kuonyesha wanapendana. Aidha, wapo ambao wanashindwa kujua namna ya kutongoza; kwa ujumla kutongoza ni uwezo wa ushawishi kwamba unamwambia mwanamke unamuhitaji na kumpenda awe wako au wakati mwingine hata mwanamke anaweza kuanza. Ndio ukweli wenyewe Sio kweli kwamba kila mwanaume anajua kutongoza. Kuna wengine hata kumsimamisha mwanamke hawezi au anaogopa. Ndio unaweza kukuta mwanamume anajikanyaga namna ya kuongea. Wapo wengine wanafikiri njia sahihi ya kutongoza ni kuhonga aidha fedha au mali nk, lakini sicho hasa wanachotaka wanawake au wanaume katika mapenzi. Maneno ya ku...

Aliyoyajibu Lulu Diva baada ya kudaiwa kuwa mapenzini na Madee

Aliyoyajibu Lulu Diva baada ya kudaiwa kuwa mapenzini na Madee April 6, 2017 kupitia U heard ya XXL ya Clouds FM staa wa Bongo Fleva Lulu Diva ameweka wazi uhusiano wake na staa mwingine wa Bongo Fleva kutoka Tip Top Connection,   Madee baada ya kuonekana mara kwa mara wakiwa pamoja. Soudy Brown aliwatafuta Madee na Lulu Diva kufahamu ukweli ambapo Madee hakupatikana kwenye simu, lakini Lulu Diva alikuwa na haya ya kujibu alipoulizwa kuhusu kutoka kimapenzi na Madee . ..>>> “Madee ni kaka yangu na nimshauri wangu halafu pia kuna wimbo wake amenishirikisha, Soudy na wewe umezidi umbea, T-shirt akivaa Madee sisi wengine hatuwezi kununua? T-shirt tumenunua sare, tumenunua siku moja.”  – Lulu Diva.

Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi

Hii Ndiyo Tafsiri sahihi Ya Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi Moja ya kitu ambacho huwa hakina kipaumbele sana katika mahusiano ya kimapenzi,  kitu ambacho kinachoitwa zawadi. Lakini ukweli ni kwamba zawadi ina maana kubwa sana katika mahusiano ya kimapenzi zaidi hata udhaniavyo. Na Katika tafiti ambazo zimewahi fanywa ni kwamba, suala zima la utoaji zawadi katika mahusiano ya kimapenzi lilimekuwa likileta hisia zaidi katika upande mmoja. Yaani hapa nikiwa na maana ya kwamba jinsia ya kike ndiyo ambayo ipo katika kusubiri zawadi kutoka kwa jinsia ya kiume. Kutoka na suala hilo ndo maana watu wengi wamekuwa hawatilii maanani suala zima la zawadi. Lakini ukweli ni kwamba kila mtu anahusika kutoa zawadi. Huenda ukawa bado nakuacha njia panda huelewi ni zawadi gani ambayo itampendeza mpenzi wako. Wala usipate tabu afisa Mipango nipo kwa ajili yako. Ipo hivi ili kujua zawadi ambayo mwezi wako anapendezwa nayo,  Unachotakiwa kukifanya ni kwamba kwa kuwa ni mpen...