Skip to main content

Mahitaji Makuu Ya Mafanikio Kwa Msaka Mafanikio

Mahitaji makuu ya mwandamu katika kuishi vyema hapa duniani anahitaji chakula,  mavazi na maradhi,  hii ni kwa mujibu ya mwalimu wangu ambaye aliwahi nifundisha miaka ya nyuma kidogo. Lakini tukiachana na mahitaji hayo,

Itakuwa ni vigumu sana kama unataka kufikia ndoto yako kama hautakuwa na vitu vifuatavyo.
1.  Lengo kuu.
Lengo kuu hutokana na malengo mengine madogo madogo. Kama ilivyo, ili iitwe bahari ni lazima bahari hiyo iweze kupokea maji kutoka vyanzo vingine vya maji kama vile vijito, mito, mabwawa na mengineyo ndipo itatokea bahari. Kwa kuona mfano huo tunaweza tuangalie mfano mwingine ambao itatusaidia kufukia lengo kuu,
kama unahitaji kuwa mfanyabiashara mkubwa unahitaji kuwa na malengo mengine madogo madogo ambayo ndiyo yatakufanya kukamilika kwa lengo hilo kuu.  Hivyo kila wakati ikumbukwe ya kwamba ni lazima uweze kuyapapalilia vyema malengo yako madogomadogo kwani ndiyo chanzo kikubwa cha kufikia mafanikio yako.
Hivyo ili uweze kuwa mwenye mafanikio makubwa kwa upande wako unahitaji kuwa na lengo kuu ambalo litakufanya uwezo kutimiza ndoto yako.
2. Sababu
Hakuna mafanikio bila ya kuwa na sababu ya kufanya kitu hicho.  Kila kitu inachokiona katika dunia hii kumbuka ya kwamba mwanzilishi wa kitu au jambo hilo alilianzisha kwa sababu maluumu.  Huwezi kusema unataka kufanya jambo fulani kama huna sababu,  kwani mafanikio ya aina hiyo utawasikia kwa majirani tu.
Hivyo kila wakati kwa kila jambo ambalo unalitaka kulifanya,  kabla ya kufanya jambo hilo kumbuka ya kwamba ni lazima utafute sababu ya kufanya jambo hilo. Kama hautapata majibu ya kufanya jambo hilo ni vyema akaliacha kulifanya, kwani kama utaamua kulifanya jambo bila ya kuwa sababu, jambo hilo litakufa tu baada ya siku chache.  Hivyo kumbuka kila kitu ambacho unakifanya au unataka kukifanya ni lazima kuwe na sababu maalumu.
3. Msukumo wa kiutendaji.
Mafanikio hayajatokea kama ajali kama hakutakuwa na msukumo wa kiutendaji juu ya jambo hilo.  Msukumo humfanya Mtendaji wa jambo hilo kuweza kutendeka kwa ufasaha kila wakati.  Hivyo kila wakati usifanye kitu kwa sababu mtu fulani amesema ufanye,  kwani kama  atafanya hivyo utakosa hamasa ya msukumo juu ya utendaji wa jambo fulani.

Hivyo kuwepo kwa lengo kuu,  sababu ya kutenda jambo na msukumo wa kiutendaji hiyo ndiyo siri kubwa iliyojificha katika kufikia ndoto ambayo unayo.  @muungwana blog

Comments

Popular posts from this blog

je wajua,zifahamu mbinu mbalimbali za kumpata mwenzi bora

KILA mtu anapenda kuwa na mwenza mzuri, mwenye kumfaa katika maisha yake. Hata hivyo kwa bahati mbaya ni kwamba wengi wanashindwa kupata wenza wazuri. Ziko sababu nyingi lakini kubwa ni uwezo wa mtu wa kumtambua mwingine na kujua kama ni kweli anafaa au anafaa  kuendana nae au la.Wakati wa uchumba, wengi wa watu huonekana kutumiana kadi, zawadi na mambo mengine  mbalimbali yenye lengo la kuonyesha wanapendana. Aidha, wapo ambao wanashindwa kujua namna ya kutongoza; kwa ujumla kutongoza ni uwezo wa ushawishi kwamba unamwambia mwanamke unamuhitaji na kumpenda awe wako au wakati mwingine hata mwanamke anaweza kuanza. Ndio ukweli wenyewe Sio kweli kwamba kila mwanaume anajua kutongoza. Kuna wengine hata kumsimamisha mwanamke hawezi au anaogopa. Ndio unaweza kukuta mwanamume anajikanyaga namna ya kuongea. Wapo wengine wanafikiri njia sahihi ya kutongoza ni kuhonga aidha fedha au mali nk, lakini sicho hasa wanachotaka wanawake au wanaume katika mapenzi. Maneno ya ku...

Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi

Hii Ndiyo Tafsiri sahihi Ya Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi Moja ya kitu ambacho huwa hakina kipaumbele sana katika mahusiano ya kimapenzi,  kitu ambacho kinachoitwa zawadi. Lakini ukweli ni kwamba zawadi ina maana kubwa sana katika mahusiano ya kimapenzi zaidi hata udhaniavyo. Na Katika tafiti ambazo zimewahi fanywa ni kwamba, suala zima la utoaji zawadi katika mahusiano ya kimapenzi lilimekuwa likileta hisia zaidi katika upande mmoja. Yaani hapa nikiwa na maana ya kwamba jinsia ya kike ndiyo ambayo ipo katika kusubiri zawadi kutoka kwa jinsia ya kiume. Kutoka na suala hilo ndo maana watu wengi wamekuwa hawatilii maanani suala zima la zawadi. Lakini ukweli ni kwamba kila mtu anahusika kutoa zawadi. Huenda ukawa bado nakuacha njia panda huelewi ni zawadi gani ambayo itampendeza mpenzi wako. Wala usipate tabu afisa Mipango nipo kwa ajili yako. Ipo hivi ili kujua zawadi ambayo mwezi wako anapendezwa nayo,  Unachotakiwa kukifanya ni kwamba kwa kuwa ni mpen...

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...