Skip to main content

Mahitaji Makuu Ya Mafanikio Kwa Msaka Mafanikio

Mahitaji makuu ya mwandamu katika kuishi vyema hapa duniani anahitaji chakula,  mavazi na maradhi,  hii ni kwa mujibu ya mwalimu wangu ambaye aliwahi nifundisha miaka ya nyuma kidogo. Lakini tukiachana na mahitaji hayo,

Itakuwa ni vigumu sana kama unataka kufikia ndoto yako kama hautakuwa na vitu vifuatavyo.
1.  Lengo kuu.
Lengo kuu hutokana na malengo mengine madogo madogo. Kama ilivyo, ili iitwe bahari ni lazima bahari hiyo iweze kupokea maji kutoka vyanzo vingine vya maji kama vile vijito, mito, mabwawa na mengineyo ndipo itatokea bahari. Kwa kuona mfano huo tunaweza tuangalie mfano mwingine ambao itatusaidia kufukia lengo kuu,
kama unahitaji kuwa mfanyabiashara mkubwa unahitaji kuwa na malengo mengine madogo madogo ambayo ndiyo yatakufanya kukamilika kwa lengo hilo kuu.  Hivyo kila wakati ikumbukwe ya kwamba ni lazima uweze kuyapapalilia vyema malengo yako madogomadogo kwani ndiyo chanzo kikubwa cha kufikia mafanikio yako.
Hivyo ili uweze kuwa mwenye mafanikio makubwa kwa upande wako unahitaji kuwa na lengo kuu ambalo litakufanya uwezo kutimiza ndoto yako.
2. Sababu
Hakuna mafanikio bila ya kuwa na sababu ya kufanya kitu hicho.  Kila kitu inachokiona katika dunia hii kumbuka ya kwamba mwanzilishi wa kitu au jambo hilo alilianzisha kwa sababu maluumu.  Huwezi kusema unataka kufanya jambo fulani kama huna sababu,  kwani mafanikio ya aina hiyo utawasikia kwa majirani tu.
Hivyo kila wakati kwa kila jambo ambalo unalitaka kulifanya,  kabla ya kufanya jambo hilo kumbuka ya kwamba ni lazima utafute sababu ya kufanya jambo hilo. Kama hautapata majibu ya kufanya jambo hilo ni vyema akaliacha kulifanya, kwani kama utaamua kulifanya jambo bila ya kuwa sababu, jambo hilo litakufa tu baada ya siku chache.  Hivyo kumbuka kila kitu ambacho unakifanya au unataka kukifanya ni lazima kuwe na sababu maalumu.
3. Msukumo wa kiutendaji.
Mafanikio hayajatokea kama ajali kama hakutakuwa na msukumo wa kiutendaji juu ya jambo hilo.  Msukumo humfanya Mtendaji wa jambo hilo kuweza kutendeka kwa ufasaha kila wakati.  Hivyo kila wakati usifanye kitu kwa sababu mtu fulani amesema ufanye,  kwani kama  atafanya hivyo utakosa hamasa ya msukumo juu ya utendaji wa jambo fulani.

Hivyo kuwepo kwa lengo kuu,  sababu ya kutenda jambo na msukumo wa kiutendaji hiyo ndiyo siri kubwa iliyojificha katika kufikia ndoto ambayo unayo.  @muungwana blog

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyin