Skip to main content

Sababu ya Yanga kuachwa na ndege

Baadhi ya wachezaji wa Yanga

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga ambao juzi walifungwa bao 4-0 katika mechi ya marudiano baina ya yanga na AC Alger kuwania nafasi ya kucheza makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Baada ya mchezo huo kuisha kwa Yanga kutolewa katika michuano hiyo, timu hiyo ilijikuta imekwama kurudi Tanzania baada ya wachezaji wake kuachwa na ndege nchini Algeria, Katibu Mkuu wa Yanga Mkwasa anasema kitendo hicho cha timu yake kuachwa na ndege ni kutokana na mawasiliano mabovu na wenyeji wao, pamoja na foleni.

"Sisi si mara ya kwanza kusafiri na usafiri huu pia kufuata ratiba tuwapo nje ya nchi . Tunauzoefu mkubwa tu na hili. Mawasiliano yetu na wenyeji wetu yamekuwa magumu kupelekea hali hii kutokea" - Alisema Boniface Mkwasa

Kwa mujibu wa taarifa ya Yanga inasema kuwa taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao kuwa walichelewa kwa uzembe wao si za kweli kwani wenyeji wao ndiyo walikuwa wazembe kwenye kukamilisha baadhi ya vitu muhimu.

"Kilichowafanya kuchelewa ni uzembe wa wenyeji wao kuwatafutia polisi wa usalama barabarani kwa ajili ya road clearance.Taarifa hii ni tofauti na habari zinazoenezwa mitandaoni kwamba msafara huo chini ya katibu mkuu umefanya uzembe binafsi kuchelewa ratiba ya ndege . Wachezaji 12 pamoja na Katibu Mkuu ndio walioachwa na ndege ya Turkish Airline"

Wachezaji walioachwa na ndege ya shirika la Emirates ni kundi la kwanza . Utaratibu umekwishafanyika kwa kupatiwa usafiri kwenye ndege nyingine ya shirika hilo kwa ajili ya kuondoka kesho au keshokutwa kulingana na ratiba .

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyin