Skip to main content

Sababu ya Yanga kuachwa na ndege

Baadhi ya wachezaji wa Yanga

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga ambao juzi walifungwa bao 4-0 katika mechi ya marudiano baina ya yanga na AC Alger kuwania nafasi ya kucheza makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Baada ya mchezo huo kuisha kwa Yanga kutolewa katika michuano hiyo, timu hiyo ilijikuta imekwama kurudi Tanzania baada ya wachezaji wake kuachwa na ndege nchini Algeria, Katibu Mkuu wa Yanga Mkwasa anasema kitendo hicho cha timu yake kuachwa na ndege ni kutokana na mawasiliano mabovu na wenyeji wao, pamoja na foleni.

"Sisi si mara ya kwanza kusafiri na usafiri huu pia kufuata ratiba tuwapo nje ya nchi . Tunauzoefu mkubwa tu na hili. Mawasiliano yetu na wenyeji wetu yamekuwa magumu kupelekea hali hii kutokea" - Alisema Boniface Mkwasa

Kwa mujibu wa taarifa ya Yanga inasema kuwa taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao kuwa walichelewa kwa uzembe wao si za kweli kwani wenyeji wao ndiyo walikuwa wazembe kwenye kukamilisha baadhi ya vitu muhimu.

"Kilichowafanya kuchelewa ni uzembe wa wenyeji wao kuwatafutia polisi wa usalama barabarani kwa ajili ya road clearance.Taarifa hii ni tofauti na habari zinazoenezwa mitandaoni kwamba msafara huo chini ya katibu mkuu umefanya uzembe binafsi kuchelewa ratiba ya ndege . Wachezaji 12 pamoja na Katibu Mkuu ndio walioachwa na ndege ya Turkish Airline"

Wachezaji walioachwa na ndege ya shirika la Emirates ni kundi la kwanza . Utaratibu umekwishafanyika kwa kupatiwa usafiri kwenye ndege nyingine ya shirika hilo kwa ajili ya kuondoka kesho au keshokutwa kulingana na ratiba .

Comments

Popular posts from this blog

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta...