Skip to main content

Sababu ya Yanga kuachwa na ndege

Baadhi ya wachezaji wa Yanga

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga ambao juzi walifungwa bao 4-0 katika mechi ya marudiano baina ya yanga na AC Alger kuwania nafasi ya kucheza makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Baada ya mchezo huo kuisha kwa Yanga kutolewa katika michuano hiyo, timu hiyo ilijikuta imekwama kurudi Tanzania baada ya wachezaji wake kuachwa na ndege nchini Algeria, Katibu Mkuu wa Yanga Mkwasa anasema kitendo hicho cha timu yake kuachwa na ndege ni kutokana na mawasiliano mabovu na wenyeji wao, pamoja na foleni.

"Sisi si mara ya kwanza kusafiri na usafiri huu pia kufuata ratiba tuwapo nje ya nchi . Tunauzoefu mkubwa tu na hili. Mawasiliano yetu na wenyeji wetu yamekuwa magumu kupelekea hali hii kutokea" - Alisema Boniface Mkwasa

Kwa mujibu wa taarifa ya Yanga inasema kuwa taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao kuwa walichelewa kwa uzembe wao si za kweli kwani wenyeji wao ndiyo walikuwa wazembe kwenye kukamilisha baadhi ya vitu muhimu.

"Kilichowafanya kuchelewa ni uzembe wa wenyeji wao kuwatafutia polisi wa usalama barabarani kwa ajili ya road clearance.Taarifa hii ni tofauti na habari zinazoenezwa mitandaoni kwamba msafara huo chini ya katibu mkuu umefanya uzembe binafsi kuchelewa ratiba ya ndege . Wachezaji 12 pamoja na Katibu Mkuu ndio walioachwa na ndege ya Turkish Airline"

Wachezaji walioachwa na ndege ya shirika la Emirates ni kundi la kwanza . Utaratibu umekwishafanyika kwa kupatiwa usafiri kwenye ndege nyingine ya shirika hilo kwa ajili ya kuondoka kesho au keshokutwa kulingana na ratiba .

Comments

Popular posts from this blog

je wajua,zifahamu mbinu mbalimbali za kumpata mwenzi bora

KILA mtu anapenda kuwa na mwenza mzuri, mwenye kumfaa katika maisha yake. Hata hivyo kwa bahati mbaya ni kwamba wengi wanashindwa kupata wenza wazuri. Ziko sababu nyingi lakini kubwa ni uwezo wa mtu wa kumtambua mwingine na kujua kama ni kweli anafaa au anafaa  kuendana nae au la.Wakati wa uchumba, wengi wa watu huonekana kutumiana kadi, zawadi na mambo mengine  mbalimbali yenye lengo la kuonyesha wanapendana. Aidha, wapo ambao wanashindwa kujua namna ya kutongoza; kwa ujumla kutongoza ni uwezo wa ushawishi kwamba unamwambia mwanamke unamuhitaji na kumpenda awe wako au wakati mwingine hata mwanamke anaweza kuanza. Ndio ukweli wenyewe Sio kweli kwamba kila mwanaume anajua kutongoza. Kuna wengine hata kumsimamisha mwanamke hawezi au anaogopa. Ndio unaweza kukuta mwanamume anajikanyaga namna ya kuongea. Wapo wengine wanafikiri njia sahihi ya kutongoza ni kuhonga aidha fedha au mali nk, lakini sicho hasa wanachotaka wanawake au wanaume katika mapenzi. Maneno ya ku...

Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi

Hii Ndiyo Tafsiri sahihi Ya Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi Moja ya kitu ambacho huwa hakina kipaumbele sana katika mahusiano ya kimapenzi,  kitu ambacho kinachoitwa zawadi. Lakini ukweli ni kwamba zawadi ina maana kubwa sana katika mahusiano ya kimapenzi zaidi hata udhaniavyo. Na Katika tafiti ambazo zimewahi fanywa ni kwamba, suala zima la utoaji zawadi katika mahusiano ya kimapenzi lilimekuwa likileta hisia zaidi katika upande mmoja. Yaani hapa nikiwa na maana ya kwamba jinsia ya kike ndiyo ambayo ipo katika kusubiri zawadi kutoka kwa jinsia ya kiume. Kutoka na suala hilo ndo maana watu wengi wamekuwa hawatilii maanani suala zima la zawadi. Lakini ukweli ni kwamba kila mtu anahusika kutoa zawadi. Huenda ukawa bado nakuacha njia panda huelewi ni zawadi gani ambayo itampendeza mpenzi wako. Wala usipate tabu afisa Mipango nipo kwa ajili yako. Ipo hivi ili kujua zawadi ambayo mwezi wako anapendezwa nayo,  Unachotakiwa kukifanya ni kwamba kwa kuwa ni mpen...

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...