Skip to main content

Mambo Ya Kuzingatia Pale Unapoanzisha Biashara

Njia pekee itakuyokusaidia kuingiza kipato cha ziada na kukupeleka kwenye uhuru wa kifedha ni kwa wewe kuamua kuanzisha biashara yako na utakayoamua kuisimamia kikamilifu hadi ikuletee mafanikio.

Ili kuanzisha biashara na ikafika mahali ukaanza kuona matunda ya biashara yako, kwa kawaida huwa ipo misingi au mambo ambayo unatakiwa uzingatie sana ili biashara yako iweze kudumu na kutoa faida uitakayo.

Yafuatayo Ni Mambo Ya Kuzingatia Pale Unapoanzisha Biashara.
 1. Elewa wateja wako wa mwanzo wanataka nini na hapo utapata picha ya jinsi utavyoiendesha biashara na uzingativu juu ya kazi. Ukijua wateja wako wanataka kitu gani, itakusaidia sana kuweza kuwapa huduma hiyo.

2. Kuwa mbunifu,  hilo ndilo jambo kubwa zaidi, biashara ni zilezile ila kinachofanya wateja wakimbilie biashara  yako ni ubunifu wako. Kama usipokuwa mbunifu na ukataka kufanikiwa kibiashara uwe na uhakika utakwama.

3. Lugha nzuri kwa wateja na ukarimu, huweza kumasisha kuongezeka wa wateja wengi katika biashara yako. hakua biashara ambayo italeta mafanikio makubwa kama wewe mwenyewe una lugha mbovu na wateja wako.

4. Epuka kutoa pesa ya mtaji kwa mahitaji binafsi utaua biashara. Hakikisha mahitaji ya biashara na mahitaji yako binafsi unatenga kabisa. ni sumu kubwa sana katika biashara kama eti huwezi kutofautisha matumizi binafsi  na biashara yako.

5. Jenga utaratibu wa  kufanya tathimi ya biashara yako wapi ulipotokana wapi ulipo na wap unaelekea,? Je, unasonga mbele au unarudi nyuma, ukiona unarudi nyuma jiangalie upya, kujitathimini na ushituke mapema kabla jahazi halijazama.

6. Hifadhi kumbukumbu, hasa matumizi pamoja na mapato hata ya shilingi moja ya sehem ya biashara. Jambo ambalo watu wengi hasa sisi weusi ni ngumu kwetu, na hii ni kila siku unatakiwa kufanya. Huwezi kuendesha biashara na  ikakua bila ‘documentation’. Hutajua ulikotoka, ulipo na unako enda kibiashara.

7. Kujifunza kutoka kwa watu mbalimbali wanaofanya biashara kama yako na kufanikiwa pia usiwapuuze walioshindwa kwani nao wanacho cha kukufundisha. Jifunze kwao kila siku hadi uweze kufanikiwa.

8. Kuhakikisha biashara/duka haliishiwi bidhaa na kama likiishiwa bidhaa maana yake uliowakopesha hawajarudisha, pia jitahidi kuweka mambo, mazingira ya kuvutia wateja. Ukiweka mazingira hayo ujue ni lazima utaweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa.

9. Kujitahidi kuweka aina ya bidhaa ambazo wateja wako watapata kwa urahisi na jamii itakayo kuzunguka. Mteja anapenda sana duka ambalo kila akienda hakosi bidhaa ambayo anaihitaji. Hapo ndipo mahali pake.

10. Jitahidi na jifunze kukubali challenges/changamoto  katika biashara yako na kutafuta njia madhubuti ya kuzimaliza au kuzishughulikia. Ukiwa mtu wa kulia na hutaki changamoto uwe na uhakika hutafika popote.

11. Jitahidi kuangalia mbele kadri unavyona faida inaongezeka, jitahidi kuongeza mtaji na kuzid kupanua biashara, hata kwa kufungua matawi zaidi pengine na kuongeza ubora na ufanisi.

12. Usafi, ukarimu, kusoma nyakati, utafiti na ubunifu na ni moja pia ya mambo ya kuzingatia. Eneo lako la biashara likiwa safi na ukaongeza na ukarimu ni lazima utawavuta wateja wako katika biashara kwa sehemu kubwa.

Kama unataka kuanzisha biashara na ikakupa faida, hayo ndiyo mambo ya msingi sana unatakiwa kuyazingatia na kuyatilia maanani kwa kiasi kikubwa ili kupata mafanikio makubwa katika biashara yako.
 Habari @ muungwa.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta...

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as...

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...