Skip to main content

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini


Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra.
Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho.

''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo.

Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya.

Mara kadhaa maisha yetu yamekuwa ni yale yale kwa asilimia kubwa hii ni kutokana na uongo ambao kila mmoja aweka ndani ya nafsi yake, na uongo huo huo bila kujali kama una madhara makubwa katika maisha yetu ndio tumekuwa tukiusujudu kwa namna moja ama nyingine.

Unajua binadamu huongozwa kwa asilimia kubwa na mtazamo, mtazamo huo huo umegawanyika katika makundi mawili hapa nina maanisha mtazamo chanya na mtazamo hasi.

Na pia kama unaamini katika kujifunza kama mimi utagundua ya kwamba watu wengi ambao wamefanikiwa, watu hao kwa kiwango kikubwa huwa na mtazamo chanya sana. Lakini ni kwanini watu wengi ambao hatupo katika mtazamo chanya maisha yetu daima yapo vilevile ?
Hii ni kutokana tumezoea kufanya vitu kawaida kwa njia ile moja huku tukiamini mafanikio yanakuja kwakufanya hivyo. Kufanya hivyo ni kuendelea kujidanganya.

Wito wangu kwako kama nilivyoanza hapo juu tuache kujidanganya wenyewe kama kweli tunataka mafanikio . Huenda tangu hapo juu hadi nilipofikia hujanielewa mtu huwa anajidanganyaje? Shusha pumzi kidogo huku na mimi nikizidi kutumia halmashauri yangu ya kichwa na mamlaka ya mkono kukujuza zaidi kama ifuatavyo.
Binadamu ni kiumbe wa kujifajiri sana hata sehemu isiyo farijika unashangaa wala usishange afisa mipango nakandamiza kwa kupaka wino mweusi kwa kusema huo ndio ukweli.

Tujikite japo kwa sekunde chache japo ni nyingi kimaana katika kuuleza yafuatayo, tuangalie wafanyabiashara wangapi ambao hutumia vinywa vyao katika kuzidanganya nafsi zao ambazo huwa zinaathiri mafanikio yao kwa ujumla?

Ukijaribu kumuuliza mtu ambaye anafanya biashara kwamba biashara yake inaendeleaje? Hata kama biashara hiyo haiendi vizuri kiasi gani atakwambia biashara ni nzuri, mmh huku ndiko kujifariji kwenyewe, kwanini tusiwe wakweli wa nafsi zetu.

Hebu taangalie wale ambao ni wasomi ambao bado wanatumia kalamu zao katika kupata ujuzi zaidi, na hao hao ukiwauliza unaendeleaje na masomo hata kama anafeli kwa kiasi gani katika masomo yake utamsikia msomi huyo huyo atakwambia naendelea vizuri, aah tunakwenda wapi kwa kujifajiri kwa vitu ambavyo vimekuwa havitusaidii hata chembe zaidi kuendelea kufeli?
Siku zote tuache kujifariji kwa kuwadandanya wengine ya kwamba tunaendelea vizuri wakati uhalisia wake hauko hivo.

Kuendelea kujidanganya wenyewe. binafsi ni sawa na kutumia muwa kama fimbo ya kutembea kwani utafika mahali utautafuna tu.
Inawezekana pia licha kuendelea kuidanganya nafsi yako kwa namna moja ama nyingine, umekuwa ukiitumia fimbo hiyo hiyo kuwafariji wengine na huku kufanya hivyo unahisi kutamsaidia mtu huyo kumbe ukweli na uhalisia wake haupo hivyo hata chembe.

Kuna usemi fulani ulikuja kwa ndege unaseme ''the only truth shall set you free" kwa kibantu ukiwa na maana "ukweli pekee ndio utaokuweka huru" haina haja ya kuinua macho angani kutafakari katika kujua msemo huo maana unajieleza kabisa na upo wazi kwa maana unaeleweka kabisa.

Kuanzia sasa badili mtazamo wako kwa kuwa na fikra chanya ambayo itakufanya ujisemee ukweli, wewe binafsi na watu wengine kwani kufanya hivi kutakupa uhuru mkubwa kwa jambo ambalo unalifanya na huku matokeo ya kimafanikio yakija kwa upande wako kwa asilimia kubwa zaidi. Pia tuwakumbuke wahenga ambao wazidi kutupa hamasa kwa kusema hatma ya maisha yako unayo wewe mwenyewe.

Ni matumaini yangu makubwa unakwenda kubadilikia kuanzia sasa na mafanikio makubwa yatakwenda kuwa ukweli endapo utakwenda kuchukua hatua madhubuti zenye matokeo chanya.

Comments

Popular posts from this blog

je wajua,zifahamu mbinu mbalimbali za kumpata mwenzi bora

KILA mtu anapenda kuwa na mwenza mzuri, mwenye kumfaa katika maisha yake. Hata hivyo kwa bahati mbaya ni kwamba wengi wanashindwa kupata wenza wazuri. Ziko sababu nyingi lakini kubwa ni uwezo wa mtu wa kumtambua mwingine na kujua kama ni kweli anafaa au anafaa  kuendana nae au la.Wakati wa uchumba, wengi wa watu huonekana kutumiana kadi, zawadi na mambo mengine  mbalimbali yenye lengo la kuonyesha wanapendana. Aidha, wapo ambao wanashindwa kujua namna ya kutongoza; kwa ujumla kutongoza ni uwezo wa ushawishi kwamba unamwambia mwanamke unamuhitaji na kumpenda awe wako au wakati mwingine hata mwanamke anaweza kuanza. Ndio ukweli wenyewe Sio kweli kwamba kila mwanaume anajua kutongoza. Kuna wengine hata kumsimamisha mwanamke hawezi au anaogopa. Ndio unaweza kukuta mwanamume anajikanyaga namna ya kuongea. Wapo wengine wanafikiri njia sahihi ya kutongoza ni kuhonga aidha fedha au mali nk, lakini sicho hasa wanachotaka wanawake au wanaume katika mapenzi. Maneno ya ku...

Aliyoyajibu Lulu Diva baada ya kudaiwa kuwa mapenzini na Madee

Aliyoyajibu Lulu Diva baada ya kudaiwa kuwa mapenzini na Madee April 6, 2017 kupitia U heard ya XXL ya Clouds FM staa wa Bongo Fleva Lulu Diva ameweka wazi uhusiano wake na staa mwingine wa Bongo Fleva kutoka Tip Top Connection,   Madee baada ya kuonekana mara kwa mara wakiwa pamoja. Soudy Brown aliwatafuta Madee na Lulu Diva kufahamu ukweli ambapo Madee hakupatikana kwenye simu, lakini Lulu Diva alikuwa na haya ya kujibu alipoulizwa kuhusu kutoka kimapenzi na Madee . ..>>> “Madee ni kaka yangu na nimshauri wangu halafu pia kuna wimbo wake amenishirikisha, Soudy na wewe umezidi umbea, T-shirt akivaa Madee sisi wengine hatuwezi kununua? T-shirt tumenunua sare, tumenunua siku moja.”  – Lulu Diva.

Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi

Hii Ndiyo Tafsiri sahihi Ya Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi Moja ya kitu ambacho huwa hakina kipaumbele sana katika mahusiano ya kimapenzi,  kitu ambacho kinachoitwa zawadi. Lakini ukweli ni kwamba zawadi ina maana kubwa sana katika mahusiano ya kimapenzi zaidi hata udhaniavyo. Na Katika tafiti ambazo zimewahi fanywa ni kwamba, suala zima la utoaji zawadi katika mahusiano ya kimapenzi lilimekuwa likileta hisia zaidi katika upande mmoja. Yaani hapa nikiwa na maana ya kwamba jinsia ya kike ndiyo ambayo ipo katika kusubiri zawadi kutoka kwa jinsia ya kiume. Kutoka na suala hilo ndo maana watu wengi wamekuwa hawatilii maanani suala zima la zawadi. Lakini ukweli ni kwamba kila mtu anahusika kutoa zawadi. Huenda ukawa bado nakuacha njia panda huelewi ni zawadi gani ambayo itampendeza mpenzi wako. Wala usipate tabu afisa Mipango nipo kwa ajili yako. Ipo hivi ili kujua zawadi ambayo mwezi wako anapendezwa nayo,  Unachotakiwa kukifanya ni kwamba kwa kuwa ni mpen...