Skip to main content

Jinsi Masaju, Jenista walivyohangaika na Lissu bungeni

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na wenye Ulemavu), Jenista Mhagama na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju jana walikuwa na kazi ya ziada ya kumwongoza Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa Wizara ya Katiba na Sheria, Tundu Lissu kuisoma hotuba yake iliyoonekana kuwa na dosari kutokana na kuwa na maneno yenye ukakasi.

Hali hiyo iliibuka baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kumwita Lissu kuwasilisha hotuba yake. Kabla ya kuanza kusoma, Jenista ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Serikali alimuomba Mwenyekiti kuizuia hotuba hiyo kwa kuwa imejaa maneno ambayo masuala yake yapo mahakamani na pia amezungumzia mwenendo wa Rais, jambo ambalo ni kinyume cha Kanuni za Bunge.

Alisema hotuba hiyo ina mambo mengi yanayokiuka kanuni. Alisema katika hotuba hiyo kuna mambo ya mienendo ya kesi ambazo zipo mahakamani, jambo ambalo ni kinyume na kanuni na pia, kuna mambo yanayozungumzia mwenendo wa Rais, jambo ambalo ni kinyume cha Kanuni Kifungu 64 (1) (e). “Naomba nitoe utaratibu ni kwanini hoja hii irudishwe mezani kwako na maeneo yanayokiuka kanuni hizi yaweze kuondolewa na ndipo iweze kuwasilishwa ndani ya Bunge hili,” alisema Waziri Mhagama.

Hata hivyo, Chenge alimruhusu Lissu kusoma hotuba yake huku akimtaka Waziri Mhagama kuainisha maeneo yaliyokuwa na maneno yenye ukakasi. Wakati huo Lissu alianza kusoma hotuba yake, lakini Chenge alimkatisha na kumtaka kuyafuta maneno hayo, kwa kuwa hayapo kwenye hotuba yake na kumtaka kwenda moja kwa moja kwenye hotuba.

Akisoma hotuba hiyo, Lissu alisema hiyo ni mara yake ya saba kusimama mbele ya Bunge kutoa maoni ya kambi rasmi ya upinzani kuhusu Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria na ameshangaa kuona Wizara hiyo imekuwa ikiongoza kwa kuwa na mabadiliko mengi ya mawaziri kuliko wizara nyingine. Alisema baada ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2010, alianza Celina Kombani (sasa marehemu) kisha wakafuata Mathias Chakawe, Dk Asha-Rose Migiro, Dk Harrison Mwanyembe na sasa Profesa Palamagamba Kabudi.

Alisema ingawa Profesa Kabudi anaweza kuwa mgeni bungeni, lakini si katika uelewa wa matatizo makubwa ya kisiasa na kikatiba nchini. Alimkumbusha majukumu makubwa na mazito anayolazimika kuyabeba kwa nafasi yake hiyo. @muungwana.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyin