Skip to main content

Tanzania imeng'ara viwango vya FIFA

Tanzania imeng'ara viwango vya FIFA, imepanda Kwa nafasi 22

TANZANIA imepanda Kwa nafasi 22 kwenye viwango vya FIFA duniani kutoka nafasi ya 157 kwa mwezi wa pili na sasa imeshika namba135. Hii inatokana na Stars kufanya vizuri kwenye mechi mbili za kirafiki dhidi ya Botswana waliyoshida kwa magoli 2-0 na Burundi iliyoshinda kwa magoli 2-1.
Pia Brazil imeipiku Argentina kwenye nafasi ya kwanza kwa mwezi wa tatu Argentina ilikuwa nafasi ya kwanza kwa mwezi wa pili huku Brazil wakiwa nafasi ya pili. Haya ndio mataifa kumi yanayoongoza kwenye viwango vya soka Duniani 1. Brazil 2. Argentina 3. Germany 4. Chile 5. Colombia 6. Ufaransa 7. Ubeligiji 8. Ureno 9. Uswisi na 10. Hispania.
Mataifa 10 yanayongoza Afrika, kwenye mabano ni nafasi zao za viwango vya ubora duniani.
1. Misri (19) 2. Senegal (30) 3.C ameroon (33) 4. Burkinafaso (35) 5. Nigeria (40) 6. DR Congo (41) 7. Tunisia (42) 8. Ghana (45) 9. Ivory Coast (48) 10. Morocco (53)
Kwa Afrika Mashariki Uganda inaendelea kuongoza ikiwa nafasi 72 ikiwa imepanda nafasi 3 kutoka 75 ya mwezi wa Pili, Kenya nafasi 78 nayo ikiwa imepanda Kwa nafasi 10 kutoka 88 ya Mwezi uliopita wakati Rwanda yenyewe inakamata nafasi ya 117 ikiwa imeshuka kwa nafasi 17 kutoka nafasi ya 100 ya mwezi uliopita na Burundi ambao ilifungwa na Tanzania ipo katika nafasi ya 141 nayo ikiwa imeporomoka kwa nafasi 3 kutoka nafasi ya 138 ya mwezi wa pili

Comments

Popular posts from this blog

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...

KILIMO CHA KISASA CHA MPUNGA

Utangulizi Mpunga ni zao la pili la chakula kwa umuhimu linalolimwa sehemu nyingi nchini Tanzania. Umuhimu wa zao hili umeongezeka kuanzia muongo uliopita kutokana na jamii za mijini na vijijini kupendelea zaidi kula wali na kupunguza ulaji wa vyakula vingine na kulifanya zao hili kuwa la chakula na biashara. Mvua ni chanzo kikuu cha maji kwenye kilimo cha mpunga. Viwango vya mahitaji ya maji katika kukua kwa mpunga hutofautiana miongoni mwa aina za mpunga. Ni kwa jinsi hii mpunga hupandwa katika mazingira mbalimbali kutegemea na mahitaji yake ya maji. Zipo aina tatu kuu za mazingira yanayolimwa mpunga kulingana na upatikanaji wa maji na hali ya mwinuko wa nchi. Mazingira haya ni kilimo cha mpunga wa mabondeni kinachotegemea mvua (72%), kilimo cha mpunga wa kwenye miinuko (20%) na kilimo cha mpunga cha umwagiliaji (8%). Kiasi cha mpunga kinachozalishwa nchini kimekuwa kikiongezeka mwaka hadi mwaka kutoka tani 41,000 mwaka 1970 hadi tani 811,500 mwaka 1998. Ongezeko hi...