Skip to main content

Tanzania imeng'ara viwango vya FIFA

Tanzania imeng'ara viwango vya FIFA, imepanda Kwa nafasi 22

TANZANIA imepanda Kwa nafasi 22 kwenye viwango vya FIFA duniani kutoka nafasi ya 157 kwa mwezi wa pili na sasa imeshika namba135. Hii inatokana na Stars kufanya vizuri kwenye mechi mbili za kirafiki dhidi ya Botswana waliyoshida kwa magoli 2-0 na Burundi iliyoshinda kwa magoli 2-1.
Pia Brazil imeipiku Argentina kwenye nafasi ya kwanza kwa mwezi wa tatu Argentina ilikuwa nafasi ya kwanza kwa mwezi wa pili huku Brazil wakiwa nafasi ya pili. Haya ndio mataifa kumi yanayoongoza kwenye viwango vya soka Duniani 1. Brazil 2. Argentina 3. Germany 4. Chile 5. Colombia 6. Ufaransa 7. Ubeligiji 8. Ureno 9. Uswisi na 10. Hispania.
Mataifa 10 yanayongoza Afrika, kwenye mabano ni nafasi zao za viwango vya ubora duniani.
1. Misri (19) 2. Senegal (30) 3.C ameroon (33) 4. Burkinafaso (35) 5. Nigeria (40) 6. DR Congo (41) 7. Tunisia (42) 8. Ghana (45) 9. Ivory Coast (48) 10. Morocco (53)
Kwa Afrika Mashariki Uganda inaendelea kuongoza ikiwa nafasi 72 ikiwa imepanda nafasi 3 kutoka 75 ya mwezi wa Pili, Kenya nafasi 78 nayo ikiwa imepanda Kwa nafasi 10 kutoka 88 ya Mwezi uliopita wakati Rwanda yenyewe inakamata nafasi ya 117 ikiwa imeshuka kwa nafasi 17 kutoka nafasi ya 100 ya mwezi uliopita na Burundi ambao ilifungwa na Tanzania ipo katika nafasi ya 141 nayo ikiwa imeporomoka kwa nafasi 3 kutoka nafasi ya 138 ya mwezi wa pili

Comments

Popular posts from this blog

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta...