Skip to main content

Posts

Showing posts from April, 2017

Genk Yaua 3-0 Kufuzu Ulaya, Samatta atokea benchi

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta jana ametokea benchi KRC Genk ikiibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya Kortrijk kwenye mchezo wa Kundi B kuwania tiketi ya kucheza michuano ya UEFA Europa League mwakani. Samatta aliingia dakika ya 66 kwenda kuchukua nafasi ya mfungaji wa bao la kwanza la Genk jana, kinda Mbelgiji, LeandroTrossard aliyefunga kwa penalti dakika ya 14 katika mchezo huo ambao mabao mengine yalifungwa na kinda mwingine Mbelgiji, Siebe Schrijvers mawili, dakika ya 45 na 70. Samatta alianzia benchi jana baada ya mchezo uliopita kuanzishwa Jumatano, lakini hakufunga KRC Genk wakilazimishwa sare ya 1-1 na wenyeji, AS Eupen Uwanja wa Kehrweg mjini. Genk inaendelea kuongoza Kundi B katika mchuano wa kuwania tiketi ya Europa League kwa pointi zake 16 sasa baada ya kucheza mechi sita na Samatta jana ameiichezea Genk mechi ya 55 tangu ajiunge nayo Januari mwaka jana kutoka TP Mazembe ya DRC akiwa amefunga mabao 18. Kati ya mechi hizo 55, mi

Sasa Wenye sifa kuchekelea ajira

Dar es Salaam. Baada ya Rais John Magufuli kuagiza watumishi waliobainika kutumia vyeti vya kughushi waondoke katika maeneo yao ya kazi mara moja kabla hawajaadhibiwa kwa mujibu wa sheria, imeelezwa kuwa hiyo inaweza kuwa neema kwa vijana wasomi wasiokuwa na ajira. Rais Magufuli alisema hayo alipokuwa akipokea ripoti ya uhakiki wa vyeti feki mjini Dodoma baada ya kukamilika kwa uhakiki uliofanyika kwa miezi sita na watumishi 9,932 wakigundulika kutumia vyeti feki huku wengine 1,538 wakitumia cheti kimoja kwa zaidi ya mtu mmoja. Akizungumzia suala hilo Mwenyekiti wa Umoja wa Maofisa Watendaji Wakuu wa Kampuni Binafsi nchini (CEOrt), Ali Mufuruki amesema kwa kufanya hivyo Serikali inaweka viwango bora vya elimu. Pia, amesema inatoa nafasi kwa waliokuwa na elimu bora angalau kuingia kwenye soko la ajira, kwa sababu kuna nafasi zipo wazi zinazotakiwa kujazwa na wale tu wenye sifa.  “Hii ni alarm hata kwa sisi sekta binafsi, kuliangalia hili kwa kina na kuongeza umakini

Sakata la vyeti feki lazua mjadala

Wasomi wamepinga kufanyika kwa ubaguzi wa wenye vyeti feki kwa kuwaacha baadhi ya mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya katika uhakiki huo. Kauli hiyo imekuja siku moja  baada ya Rais John Magufuli kuagiza wafanyakazi 9,932 waliobainika kuwa na vyeti feki, waondolewe kazini. Uamuzi huo wa Serikali umesaidia kunusuru kutumika kwa fedha nyingi kuwalipa watu wasiokuwa na sifa. Kama watumishi hao wote wanalipwa kiwango cha kima cha chini cha mshahara cha Sh300,000 jumla ya Sh35.7 bilioni zimekuwa zikitumika kila mwaka kuwalipa. Wakati akikabidhi orodha hiyo juzi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah  Kairuki amesema kazi hiyo haikuwagusa mawaziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kwa kuwa wao wanatakiwa kujua kusoma na kuandika. Kauli hiyo imeibua mjadala mzito kwa kile kilichodaiwa inalenga kutetea uovu na kuhalalisha  mambo yasiyofaa bila kuangalia wakati uliopo. Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM), Bashiru

Matano ya Ray Kigosi kwa Diamond na Kanumba kudaiwa kuwa Freemason

By   Victor Kileo TZA   on April 26, 2017 Muigizaji staa wa Bongo movie  Ray Kigosi  ni miongoni mwa mastaa wa Tanzania waliopata mafanikio makubwa kwenye industry ya filamu nchini na kufanikiwa kujijengea jina na heshima kwa jamii. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ray ametoa ujumbe ambao unalenga kutoa uelewa kwa mashabiki hasa wa filamu na muziki nchini ambao wamekuwa wakiwahusisha baadhi ya mastaa wanaofanya vizuri na imani tofauti. Katika kuufikisha ujumbe huo Ray amewatolea mfano staa wa Bongo Fleva Diamond Platnumz na muigizaji nyota Stiven Kanumba aliyefariki miaka mitano iliyopita ambaye alifanya vizuri kwenye tasnia ya Bongo movie. Ray Kigosi ameandika… 1. Kanumba alipoanza kuona mwanga wa kufanikiwa bila kujali juhudi zake kuna watu walimuita Freemanson, Mara anatumia nguvu za Giza. that is to say films zake hazikuwa nzuri but ziliuza sababu ya nguvu za Freemanson na nguvu za g

Jinsi Masaju, Jenista walivyohangaika na Lissu bungeni

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na wenye Ulemavu), Jenista Mhagama na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju jana walikuwa na kazi ya ziada ya kumwongoza Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa Wizara ya Katiba na Sheria, Tundu Lissu kuisoma hotuba yake iliyoonekana kuwa na dosari kutokana na kuwa na maneno yenye ukakasi. Hali hiyo iliibuka baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kumwita Lissu kuwasilisha hotuba yake. Kabla ya kuanza kusoma, Jenista ambaye pia ni Mnadhimu Mkuu wa Serikali alimuomba Mwenyekiti kuizuia hotuba hiyo kwa kuwa imejaa maneno ambayo masuala yake yapo mahakamani na pia amezungumzia mwenendo wa Rais, jambo ambalo ni kinyume cha Kanuni za Bunge. Alisema hotuba hiyo ina mambo mengi yanayokiuka kanuni. Alisema katika hotuba hiyo kuna mambo ya mienendo ya kesi ambazo zipo mahakamani, jambo ambalo ni kinyume na kanuni na pia, kuna mambo yanayozungumzia mwenendo wa Rais, jambo ambalo ni kin

Kipigo cha Barcelona kwa Real Madrid kilichovunja rekodi ya Real Madrid

Baada ya kuondolewa katika michuano ya UEFA Champions League kwa timu ya FC Barcelona usiku wa April 23 2017 walisafiri hadi katika jiji la Madrid kuendeleza harakati zao za kuwania Kombe la LaLiga kwa kucheza dhidi ya wapinzania wao wa jadi Real Madrid katika uwanja wa Santiago Bernabeu . Mastaa wa zamani wa Real Madrid Ronaldo de Lima na Luis Figo walikuwepo uwanjani kuangalia game. FC Barcelona walisafiri kuelekea Madrid tayari wakiwa wanamkosa mchezaji wao wa kimataifa wa Brazil Neymar kutokana na kutumikia adhabu ya kufungiwa mechi tatu, licha ya kumkosa Neymar safu ya ushambuliaji ya Barcelona  bado ilikuwa imara na kupelekea kupata ushindi wa magoli 3-2. Lionel Messi akifunga goli lake la 500 akiitumikia FC Barcelona Lionel Messi ndio ameonekana kuwa hatari zaidi kwa kumsababishia Sergio Ramos kupata kadi nyekundu ya 22 katika historia yake ya soka kutoka na kumchezea Lionel Messi  faulo dakika ya 77, L

Ufugaji Bora Wa Sungura

UTANGULIZI Kabla hujaamua kufuga sungura hakikisha ya kwamba umejitoa na una muda wa kuwahudumia wanyama waha, ufugaji wao si rahisi kama vile ukifuga paka au mbwa, sungura wanahitaji uangalizi na hassa kwenye usafi kwa sababu ni rahisi kwao kupata maradhi yatokanayo na mazingira mabaya na machafu. MABANDA Kuna aina mbili za mabanda ya kufugia kwanza ni yale ya kuwafungia ndani muda wote bila kutoka nje na ya pili ni ile ya pili ni nusu nusu yaani wanakuwa na mabanda na wanaweza kutoka nje kwenye ua maalum, katika aina zote mbili ni muhimu kuhakikisha hakuna upenyo wa kuruhusu panya kupita kwa sababu huwa wanakula watoto wa sungura. UFUGAJI WA NDANI 1. Usitumie banda la kioo (aquarium) kwa sababu halina hewa ya kutosha na ni vigumu kusafisha 2. Sakafu ya nyavu za waya ni nzuri zaidi ila hakikisha hakuna sehemu zenye ncha kali inayoweza kuwaumiza sungura, kwani wakumia ni mpaka wapone wenyewe au umchinje kwa sababu ukitumia dawa za antibiotic sung

Hivi ndivyo Tango linavyoweza kutibu vidonda vya tumbo

Bila shaka unalifahamu kwa uzuri tunda hili la tango. Je unajua ya kwamba tunda hili ni tiba tosha kwa ajili ya kutibu vidonda vya tumbo? Kama jibu ni hapana nakusihi twende sambamba katika makala haya. Tango ni mojawapo ya tunda ambalo watu wengi huwa hawalihesabu sana kama ni miongoni mwa matunda labda kutokana na kutokuwa na ladha sana. Wapo wengine huwa hawawezi kula lenyewe labda lichanganywe katika kachumbari. Lakini pamoja na hayo tunda hili linasifika zaidi kwa kuwa na uwezo katika tiba ya matatizo mbalimbali ya kiafya ikiwa ni pamoja na tatizo la vidonda vya tumbo. Aidha, pamoja na kuwa na uwezo huo pia tunda hili limekuwa likipata sifa sana kwa kuimarisha afya ya ngozi pale ambapo mhusika atatumia kusugulia usoni. Jambo la kuzingatia; Hakikisha unakula tango ambalo lipo katika hali ya ukawaida bila kuchanganywa na kitu chochote, pia unashauriwa kula tango likiwa na maganda yake, kwani maganda ndiyo yana vitamini zaidi. Hivyo watalamu wa afya wanazidi kus

Uchaguzi mdogo wazua vurugu Ifakara

Vurugu zaibuka kwenye kituo cha  kupiga kura cha Mbasa Mlimani (wilayani Ifakara)baada ya wafuasi wa vyama vya siasa kuwania kuvamia kituo hicho ambapo jeshi la Polisi lilizamika kurusha mabomu ya machozi ili kuzibiti hali hiyo. Inadaiwa kuwa virugu hizo zilitokana na uchgauzi wa Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mbasa  ambapo wafuasi hao walipinga matokeo ya uchaguzi huo na kutaka   kuvamia kituo hicho. Vurugu hizo  zilisababisha askari Huruma Mkisi kujeruhiwa kwa kupigwa jiwe kichwani na mfuasi asiyefahamika na hivyo kupelekwa katika Hospitali ya Mtakatifu Francis ya Ifakara kwa ajili ya matibabu. Mashabiki hao walianza kwa kulalamikia matokeo ya uchaguzi kucheleweshwa kutangazwa na hivyo kuwatilia shaka mawakala ambao walikuwa wakibishana kuhusu idadi ya kura walizopata wagombea wao. Akitangaza matokeo, msimamizi wa Uchaguzi huo Gaston Kaputa alimtaja mshindi  wa nafasi ya mwenyekiti wa Kijiji cha Kisawila kuwa ni Shaaban Salahange wa CCM  aliyepata kura 557 aliyefuat

Kauli ya Manara baada Kufungiwa

aliyekuwa msemaji wa Klabu ya Simba haji Manara amelalamikia adhabu aliyopewa na TFF kutokana na kuhukumiwa bila ya kusikilizwa. Manara aliachia ujumbe huo kwenye akounti yakle ya mtandao wa Picha wa Instagram jana na kudai kuwa angepewa nafasi ya kusikilizwa hata hivyo  Kamati ya nidhamu imetoa fursa kwa Manara kukata rufaa kwenda ngazi za juu ikiwa hajaridhika na maamuzi yaliyotolewa.

Jokate aivuruga UVCCM ni baada ya kuteuliwa

UTEUZI wa Miss Tanzania namba mbili wa mwaka 2006, Jokate Mwegelo kuwa Kaimu Katibu wa Uhamasishaji wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, unaonekana kutaka kuivuruga jumuiya hiyo. Mjadala mkubwa umeibuka kuhusu uteuzi huo, ambapo baadhi ya wanachama na viongozi wa juu wa jumuiya hiyo wamedai kuwa haukufuata kanuni na taratibu za umoja huo. Vyanzo vya kuaminika kutoka katika umoja huo vimeliambia MTANZANIA kuwa baadhi ya viongozi wa juu wa UVCCM hawakushirikishwa katika uteuzi huo uliofanywa na kigogo mmoja wa umoja huo. Taarifa za ndani zinaeleza kuwa uteuzi huo haukushirikisha wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji wala Baraza Kuu la UVCCM, ambalo halikukutana kumthibitisha Jokate kama kanuni zinavyoelekeza. Kwa mujibu wa kanuni za jumuiya hiyo, wajumbe wa kamati ya utekelezaji hawazidi 10, ambapo miongoni mwao ni Mwenyekiti wa umoja huo Taifa, Makamu Mwenyekiti Taifa, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na mjumbe mmoja kutoka makao makuu ya chama. Wajum

Mambo Ya Kuzingatia Pale Unapoanzisha Biashara

Njia pekee itakuyokusaidia kuingiza kipato cha ziada na kukupeleka kwenye uhuru wa kifedha ni kwa wewe kuamua kuanzisha biashara yako na utakayoamua kuisimamia kikamilifu hadi ikuletee mafanikio. Ili kuanzisha biashara na ikafika mahali ukaanza kuona matunda ya biashara yako, kwa kawaida huwa ipo misingi au mambo ambayo unatakiwa uzingatie sana ili biashara yako iweze kudumu na kutoa faida uitakayo. Yafuatayo Ni Mambo Ya Kuzingatia Pale Unapoanzisha Biashara.  1. Elewa wateja wako wa mwanzo wanataka nini na hapo utapata picha ya jinsi utavyoiendesha biashara na uzingativu juu ya kazi. Ukijua wateja wako wanataka kitu gani, itakusaidia sana kuweza kuwapa huduma hiyo. 2. Kuwa mbunifu,  hilo ndilo jambo kubwa zaidi, biashara ni zilezile ila kinachofanya wateja wakimbilie biashara  yako ni ubunifu wako. Kama usipokuwa mbunifu na ukataka kufanikiwa kibiashara uwe na uhakika utakwama. 3. Lugha nzuri kwa wateja na ukarimu, huweza kumasisha kuongezeka wa wateja wengi katik

Simba SC imesitisha kufanya maandamano

Rais wa klabu ya Simba baada ya kushauriana na kamati ya utendaji ya klabu,imeamua kusitisha maandamano iliyopanga kuyafanya Jumanne ijayo, baada ya nia na dhamira njema ya serikali kutaka kushughulikia sintofahamu inayoendelea baina ya klabu na Shirikisho la Soka nchi (TFF). Ikumbukwe jana klabu yetu kupitia kwenye barua iliosainiwa na Rais wetu Evans Aveva, iliandika kwa Jeshi la Polisi nchini ikiomba kibali cha maandamano ya amani, yaliyopangwa kuhudhuriwa na viongozi,wanachama na washabiki wa klabu, kwenda Wizara inayosimamia Michezo nchini, ili kupeleleka kilio chetu juu ya TFF. Kwa namna inavyoshughulikia malalamiko ya muda mrefu na ya sasa ya klabu hii kubwa nchini. Katika barua ilioandikwa na katibu Mkuu wa Baraza la michezo nchini (BMT), Kwa niaba ya Serikali,imetutaka Shirikisho na Klabu kutafuta namna sahihi na iliyo na weledi katika kushughulikia changamoto hizi zinazoweza kuvuruga amani ya nchi. Serikali kupitia barua hiyo,imeahidi pia kutukutanisha pan

Acha Kulalamika Juu Ya Mambo Haya Kama Ukitaka Mafanikio Ya Kweli

"Hivyo ulivyo inatokana na mtazamo ulionao" usemi huu niliwahi kukutana nao siku moja katika pekuapekua zangu, usemi huu una ukweli ndani yake kwa asilimia zote uzijuazo wewe, kwa sababu maisha yako hivyo yalivyo yanataokana na mtazamo na imani ulizonazo. Watu wengi ambao hawajafanikiwa wanaamini ya kwamba mafanikio yanapatina kwa baadhi ya watu fulani, lakini dhana hii si kweli kwa sababu kila mmoja mwenye pumzi na fikra ana wajibu wakuweza kufanikiwa kwa kiwango kikubwa. Hivyo nikwambie ya kwamba mafanikio makubwa yatakuwa upande wako endapo utaacha mara moja kulalamka juu ya mambo yautayo; 1. Acha kulalamika juu ya elimu uliyonayo. Mafanikio yatakuja kwako endapo utaacha kulalamika juu ya elimu uliyonayo. Watu wengi wanalalamika eti kwa sababu ya elimu walizonazo, wengi husema mimi sina mafanikio kwa sababu sina elimu ya kotosha, au nimesoma kidogo na sina elimu ya chuo kikuu. Kiuhalisia, dhana hii haina mahusiano ya moja kwa moja na mafanikio yako, hi

Tafakari Kwa Kujifunza Mambo Haya Yatakayoboresha Maisha Yako Leo

1. Mafanikio makubwa sana utayapata kama unafanya kitu ambacho unakipenda sana toka moyoni. Ikiwa hukipendi kile unachokifanya yaani unakifanya kitu hicho kwa kujilazimisha uwe na uhakika, hutafanikiwa sana. Hivyo kila wakati pata muda wa kujiuliza je, ni kitu gani ambacho unakipenda? Kisha baada ya hapo kifanye kitu hicho kwa nguvu zote. Kumbuka siku zote mafanikio makubwa yanakuja kwa kufanya kile kitu unachokipenda. 2. Ni rahisi kufanikiwa na kupata karibu kila kitu unachokihitaji katika maisha yako ikiwa utakuwa tayari kuwasidia wengine nao kuweza kufanikiwa. Ndio maana mara nyingi watu wenye mkono wa ‘birika’ si rahisi sana kuweza kuwaona wakifikia viwango vya mafanikio makubwa. Jiulize kitu gani ulichonacho ambacho unaweza ukakitoa na kikawa msaada mkubwa kwa wengine? Kama kitu hicho unacho hebu kitoe, acha kukaa nacho tu wewe peke yako, washirikishe na wengine ili kiwe baraka kwenu wote. 3. Kama unataka kuwa TAJIRI, kila wakati hakikisha unakuwa na akili ya

KILIMO CHA KISASA CHA MPUNGA

Utangulizi Mpunga ni zao la pili la chakula kwa umuhimu linalolimwa sehemu nyingi nchini Tanzania. Umuhimu wa zao hili umeongezeka kuanzia muongo uliopita kutokana na jamii za mijini na vijijini kupendelea zaidi kula wali na kupunguza ulaji wa vyakula vingine na kulifanya zao hili kuwa la chakula na biashara. Mvua ni chanzo kikuu cha maji kwenye kilimo cha mpunga. Viwango vya mahitaji ya maji katika kukua kwa mpunga hutofautiana miongoni mwa aina za mpunga. Ni kwa jinsi hii mpunga hupandwa katika mazingira mbalimbali kutegemea na mahitaji yake ya maji. Zipo aina tatu kuu za mazingira yanayolimwa mpunga kulingana na upatikanaji wa maji na hali ya mwinuko wa nchi. Mazingira haya ni kilimo cha mpunga wa mabondeni kinachotegemea mvua (72%), kilimo cha mpunga wa kwenye miinuko (20%) na kilimo cha mpunga cha umwagiliaji (8%). Kiasi cha mpunga kinachozalishwa nchini kimekuwa kikiongezeka mwaka hadi mwaka kutoka tani 41,000 mwaka 1970 hadi tani 811,500 mwaka 1998. Ongezeko hi