Skip to main content

Wingi wa mabao Yanga wainyima Simba ubingwa

Dar es Salaam. Adui yako mwombee njaa! Ukweli wa usemi huo unadhihirishwa na rekodi nzuri ya misimu tisa ya Ligi Kuu Tanzania Bara zinazoinyima Simba nafasi ya kutwaa ubingwa msimu huu ikilinganishwa na watani wao wa jadi, Yanga.

Tangu mfumo wa Ligi Kuu ulivyobadilika mwaka 2007, Simba imeshindwa kutwaa ubingwa ilipozidiwa mabao na Yanga.

Takwimu zaibeba juu Yanga

Hadi sasa, wakati Ligi Kuu ikielekea ukingoni, Simba imebakiza mechi tatu, tayari imefunga mabao 44, ambayo ni sita pungufu ya yaliyofungwa na Yanga iliyobakiza mechi tano.

Simba ambayo katika misimu hiyo tisa imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu mara mbili pekee, ubingwa wa msimu 2009/2010 iliuchukua ikifunga mabao 50, huku Yanga ikifunga mabao 46, wakati msimu wa 2011/2012, ambao pia ilitwaa ubingwa ilifunga mabao 46 dhidi ya 41 ya Yanga.

Tofauti na Simba, Yanga imekuwa moto mkali ilipotwaa ubingwa baada ya kubeba taji hilo ilipoongoza kwa mabao na wakati mwingine ilitwaa ubingwa huo bila hata kuongoza kwa mabao hadi mwishoni mwa msimu.

Msimu wa mwaka 2010/2011, Yanga ilitwaa ubingwa ikifunga mabao 36 wakati wapinzani wao Simba walikuwa wamefunga mabao 40.

Kwa jumla, tangu mfumo wa ligi ulipobadilika miaka 10 iliyopita, Yanga imekuwa moto wa kuotea mbali kwenye upachikaji mabao dhidi ya Simba na timu nyingine zote za Ligi Kuu.

Siyo jambo la kushangaza kuiona Yanga ikitwaa ubingwa mara sita kati ya misimu tisa. Hadi sasa, timu hiyo imepachika mabao 474 kwenye ligi tangu mwaka 2007 ikilinganishwa na 409 ya Simba.

Wakati safu yake ya ushambuliaji ikifunga mabao machache ikilinganishwa na Yanga, Simba imeonekana kuyumba pia kwenye safu ya ulinzi dhidi ya Yanga. Kwenye misimu tisa iliyopita, imeruhusu mabao 181 wakati wapinzani wao wakifungwa 176.

Wana Simba waikubali Yanga

Akizungumzia nafasi ya Simba kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu, mjumbe wa kundi la marafiki wa Simba, ‘Friends of Simba’, Mulamu Ng’hambi alisema ni finyu kutokana na udhaifu wa safu ya ushambuliaji.

“Pamoja na matatizo yao, Yanga, wanafunga mabao mengi na washambuliaji wao wanaonyesha njaa ya mabao uwanjani. Amissi Tambwe, Donald Ngoma, Saimon Msuva na Obrey Chirwa, wote wanafunga.

“Sasa, sayansi ya soka ilivyo ni kwamba ili uwe bingwa lazima ufunge mabao mengi. Huwezi kujipa moyo wa kutwaa ubingwa wakati hufungi mabao,” alisema Ng’hambi. Kiungo wa zamani wa Kariakoo ya Lindi, Jemedari Said aliyewahi pia kuichezea Simba alisema kuwa kinachowaangusha Simba ni aina ya usajili ambao wamekuwa wakiufanya.


“Simba inahitaji kuwa na wachezaji waliokomaa kiakili, wenye ubora unaoendana na hadhi yake kama timu kubwa,” alisema.     Chanzo: muungwana.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...

KILIMO CHA KISASA CHA MPUNGA

Utangulizi Mpunga ni zao la pili la chakula kwa umuhimu linalolimwa sehemu nyingi nchini Tanzania. Umuhimu wa zao hili umeongezeka kuanzia muongo uliopita kutokana na jamii za mijini na vijijini kupendelea zaidi kula wali na kupunguza ulaji wa vyakula vingine na kulifanya zao hili kuwa la chakula na biashara. Mvua ni chanzo kikuu cha maji kwenye kilimo cha mpunga. Viwango vya mahitaji ya maji katika kukua kwa mpunga hutofautiana miongoni mwa aina za mpunga. Ni kwa jinsi hii mpunga hupandwa katika mazingira mbalimbali kutegemea na mahitaji yake ya maji. Zipo aina tatu kuu za mazingira yanayolimwa mpunga kulingana na upatikanaji wa maji na hali ya mwinuko wa nchi. Mazingira haya ni kilimo cha mpunga wa mabondeni kinachotegemea mvua (72%), kilimo cha mpunga wa kwenye miinuko (20%) na kilimo cha mpunga cha umwagiliaji (8%). Kiasi cha mpunga kinachozalishwa nchini kimekuwa kikiongezeka mwaka hadi mwaka kutoka tani 41,000 mwaka 1970 hadi tani 811,500 mwaka 1998. Ongezeko hi...