Skip to main content

Wingi wa mabao Yanga wainyima Simba ubingwa

Dar es Salaam. Adui yako mwombee njaa! Ukweli wa usemi huo unadhihirishwa na rekodi nzuri ya misimu tisa ya Ligi Kuu Tanzania Bara zinazoinyima Simba nafasi ya kutwaa ubingwa msimu huu ikilinganishwa na watani wao wa jadi, Yanga.

Tangu mfumo wa Ligi Kuu ulivyobadilika mwaka 2007, Simba imeshindwa kutwaa ubingwa ilipozidiwa mabao na Yanga.

Takwimu zaibeba juu Yanga

Hadi sasa, wakati Ligi Kuu ikielekea ukingoni, Simba imebakiza mechi tatu, tayari imefunga mabao 44, ambayo ni sita pungufu ya yaliyofungwa na Yanga iliyobakiza mechi tano.

Simba ambayo katika misimu hiyo tisa imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu mara mbili pekee, ubingwa wa msimu 2009/2010 iliuchukua ikifunga mabao 50, huku Yanga ikifunga mabao 46, wakati msimu wa 2011/2012, ambao pia ilitwaa ubingwa ilifunga mabao 46 dhidi ya 41 ya Yanga.

Tofauti na Simba, Yanga imekuwa moto mkali ilipotwaa ubingwa baada ya kubeba taji hilo ilipoongoza kwa mabao na wakati mwingine ilitwaa ubingwa huo bila hata kuongoza kwa mabao hadi mwishoni mwa msimu.

Msimu wa mwaka 2010/2011, Yanga ilitwaa ubingwa ikifunga mabao 36 wakati wapinzani wao Simba walikuwa wamefunga mabao 40.

Kwa jumla, tangu mfumo wa ligi ulipobadilika miaka 10 iliyopita, Yanga imekuwa moto wa kuotea mbali kwenye upachikaji mabao dhidi ya Simba na timu nyingine zote za Ligi Kuu.

Siyo jambo la kushangaza kuiona Yanga ikitwaa ubingwa mara sita kati ya misimu tisa. Hadi sasa, timu hiyo imepachika mabao 474 kwenye ligi tangu mwaka 2007 ikilinganishwa na 409 ya Simba.

Wakati safu yake ya ushambuliaji ikifunga mabao machache ikilinganishwa na Yanga, Simba imeonekana kuyumba pia kwenye safu ya ulinzi dhidi ya Yanga. Kwenye misimu tisa iliyopita, imeruhusu mabao 181 wakati wapinzani wao wakifungwa 176.

Wana Simba waikubali Yanga

Akizungumzia nafasi ya Simba kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu, mjumbe wa kundi la marafiki wa Simba, ‘Friends of Simba’, Mulamu Ng’hambi alisema ni finyu kutokana na udhaifu wa safu ya ushambuliaji.

“Pamoja na matatizo yao, Yanga, wanafunga mabao mengi na washambuliaji wao wanaonyesha njaa ya mabao uwanjani. Amissi Tambwe, Donald Ngoma, Saimon Msuva na Obrey Chirwa, wote wanafunga.

“Sasa, sayansi ya soka ilivyo ni kwamba ili uwe bingwa lazima ufunge mabao mengi. Huwezi kujipa moyo wa kutwaa ubingwa wakati hufungi mabao,” alisema Ng’hambi. Kiungo wa zamani wa Kariakoo ya Lindi, Jemedari Said aliyewahi pia kuichezea Simba alisema kuwa kinachowaangusha Simba ni aina ya usajili ambao wamekuwa wakiufanya.


“Simba inahitaji kuwa na wachezaji waliokomaa kiakili, wenye ubora unaoendana na hadhi yake kama timu kubwa,” alisema.     Chanzo: muungwana.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyin