Skip to main content

Neema Ajira zaidi za 250 Wizara ya Ardhi


SERIKALI imezidi kutangaza neema ya ajira kwa Watanzania baada ya kubainisha kuwa katika mwaka ujao wa fedha watumishi wapya 291 wataajiriwa katika Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Waziri wa wizara hiyo, William Lukuvi, aliyasema hayo bungeni mjini hapa jana alipokuwa akiwasilisha hotuba yake kuhusu utekelezaji wa bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka huu wa fedha na makadirio ya mapato na matumizi yake kwa mwaka ujao wa fedha.

Mbali na ajira hizo mpya, alisema wizara yake itatoa mafunzo kwa watumishi 70 na kuboresha ofisi zake ili kuwezesha watumishi wengi zaidi kuhamia Dodoma.

Changamoto Tano
Lukuvi alisema wizara hiyo inakabiliwa na changamoto tano ambazo ni pamoja na uratibu wa sekta ya ardhi kusimamiwa na mamlaka zaidi ya moja na upungufu wa wataalamu na vitendea kazi vinavyohitajika ili kukidhi utoaji wa huduma katika sekta ya ardhi.

Alizitaja changamoto nyingine kuwa ni kasi ya ongezeko la watu na mifugo kulinganishwa na upatikanaji wa ardhi iliyopangwa na kupimwa, ucheleweshaji wa ulipaji wa fidia stahiki kwa ardhi iliyotwaliwa kwa ajili ya matumizi ya maendeleo na uelewa mdogo wa wananchi kuhusu sera na sheria za nchi.

Ili kutekeleza majukumu yake katika mwaka ujao wa fedha, Lukuvi aliliomba Bunge kuidhinisha bajeti ya jumla ya Sh. bilioni 70.77. Kati yake, Sh. bilioni 25.4 ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Kwa mujibu wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, wizara hiyo iliidhinishiwa Sh. bilioni 61.873 kwa ajili ya bajeti yake ya mwaka huu wa fedha. Kati yake, Sh. bilioni 20 zilikuwa za maendeleo.

Akiwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu makadirio ya wizara hiyo, Waziri Kivuli wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wilfred Lwakatare, aliishauri serikali kumaliza changamoto ya migogoro ya ardhi nchini, kuitaka Mamlaka ya Mapato (TRA) kuongeza kasi ya makusanyo ya kodi ya majengo na kuhamisha ajira za sekta ya ardhi kutoka serikali za mitaa kwenda serikali kuu.

Lwakatare ambaye pia ni Mbunge wa Bukoba Mjini (Chadema), aliishauri serikali kuunda mamlaka ya kusimamia sekta ya miliki hasa za majengo makubwa, kuwafidia wananchi waliobomolewa nyumba kupisha miradi ya serikali, kutathmini gharama za nyumba zinazojengwa na Shirika la Nyumba (NHC) na kuwaagiza wakuu wa mikoa na wilaya kutoingilia majukumu ya mabaraza ya ardhi.

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyin