Skip to main content

Ukitaka Mafanikio Ya Kweli Acha Kulalamika Juu Ya Mambo Haya

"Hivyo ulivyo inatokana na mtazamo ulionao" usemi huu niliwahi kukutana nao siku moja katika pekuapekua zangu, usemi huu una ukweli ndani yake kwa asilimia zote uzijuazo wewe, kwa sababu maisha yako hivyo yalivyo yanataokana na mtazamo na imani ulizonazo.

Watu wengi ambao hawajafanikiwa wanaamini ya kwamba mafanikio yanapatina kwa baadhi ya watu fulani, lakini dhana hii si kweli kwa sababu kila mmoja mwenye pumzi na fikra ana wajibu wakuweza kufanikiwa kwa kiwango kikubwa.

Hivyo nikwambie ya kwamba mafanikio makubwa yatakuwa upande wako endapo utaacha mara moja kulalamka juu ya mambo yautayo;

1. Acha kulalamika juu ya elimu uliyonayo.
Mafanikio yatakuja kwako endapo utaacha kulalamika juu ya elimu uliyonayo. Watu wengi wanalalamika eti kwa sababu ya elimu walizonazo, wengi husema mimi sina mafanikio kwa sababu sina elimu ya kotosha, au nimesoma kidogo na sina elimu ya chuo kikuu.

Kiuhalisia, dhana hii haina mahusiano ya moja kwa moja na mafanikio yako, hii ni kwa sababu sio kila mwenye elimu amefanikiwa hivyo kwa elimu hiyohiyo ambayo unayo ni kigezo tosha juu ya mafanikio yako. Hebu tujiulize watu wengi ambao wamefanikiwa elimu zao ni kiwango gani?

2. Acha kulalamika eti hujafanikiwa kwa sababu huna bahati.
Kama nilivyoanza kueleza hapo awali ya kwamba mtazamo ndio kila kitu, imani hii ya kuendelea kuamini ya kwamba mafanikio ni bahati nakuomba uachane nayo mara moja, imani hiyo inaweza kukupoteza na ukashindwa kupata mafanikio kama utaishikilia sana.

Tambua imani kubwa juu ya mafanikio ni kwamba kila mmoja amezaliwa kwa ajili ya kufanikiwa na si vinginevyo jambo la msingi ni kwamba mara zote hakikisha unakuwa na mtazamo chanya, ubunifu, pamoja kufanya kazi kwa bidii haijalishi ni kazi ndogo au kubwa kiasi gani.

3. Acha kulalamika eti huna pesa za kutosha.
Hili ndilo kikwazo cha mafanikio ya wengi hii ni kwasababu watu wengi wamekuwa wanalalamika ya kwamba hawana pesa za kutosha ili wafanye jambo fulani, kuendelea na tabia hii ni kujiua mwenyewe kwani siku zote pesa huwa hazitoshi.

Jambo la msingi ni kuhakikisha kwa kiwango hicho cha pesa ulichonacho ni njia pekee ya kuanza kufanya jambo unalolitaka, kwani endapo utaendelea kusubiri ufikishe kiwango fulani cha pesa ndio uanze kufanya jambo fulani nakuhakikishia huwezi kufanya kamwe.

4. Acha kulalamika juu ya serikali kama kweli unataka kufanikiwa.
Maisha yako yapo mikononi mwako, hata hivyo kama kweli unaamini hili hakikisha unakuwa bora sana katika kutafuta kusudio lako katika dunia hii, nasema hivi kwa sababu watu wengi wanashindwa kufanikiwa kwa sababu wao kazi yao ni kuilaumu serikali tu.

Na watu hao wamekuwa wakifanya hivi huku siku sikizidi kwenda na wao maisha yao yamekuwa hayabadiliki,  jambo la msingi ambalo nataka kukuasa ni kwamba kila mmoja asimame kidete katika kuyapigania maisha yake ambayo yatamtengezea kesho yake bora.

Hivyo nikuache kwa kukuambia ya kwamba endapo utaendelea na tabia yako ya kulalamika ni kutengeneza maisha yako kuwa duni zaidi.

Nukuu ya siku inasema "kulalamika ni adui namba moja wa mafanikio yako"

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyin