Skip to main content

Cristiano Ronaldo Amazing Hat-Trick vs Atletico Madrid (All Goals) 2016/17





Mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid na Timu ya Taifa ya Ureno,
Cristiano Ronaldo ameendeleza ubabe wake kwa kupiga Hatrick nyingine ya
pili mfululizo usiku wa jana kunako dimba la Santiago Bernabeu wakati
timu yake ilipovaana na mahasimu wao Atletico Madrid kwenye mchezo wa
kwanza hatua ya nusu fainali, Klabu Bingwa barani Ulaya.



Real Madrid-Atletico Madrid 3-0, l'uragano Ronaldo spazza via Simeone

Cristiano Ronaldo akishangilia goli lake la pili jana usiku dhidi ya Atletico.



Ronaldo alianza makeke yake kunako dakika ya 10′ ya mchezo huo kwa
kupiga kichwa kizito kilichopelekea mlinda mlango wa Atletico Madrid
kushindwa kuhimili mpira huo na Mreno huyo kucheka na nyavu.



Mpaka mpira unaenda mapumziko Atletico walikuwa wameshatandikwa goli
moja,na kipindi cha pili mashambulizi yaliwaelemea zaidi Atletico kwani
kunako dakika ya 73,Ronaldo alipiga shuti la mbali lililomuelemea goli
kipa kabla ya goli la tatu ambalo alifunga kunako ya 86′ na kumaliza
hesabu ya magoli 3-0,Na ikiwa pia ni Hatrick ya pili ya mfululizo baada
ya ile aliyowapiga Bayern Munich.



Ronaldo kwa sasa anakuwa ndiyo mchezaji mwenye magoli mengi zaidi kwenye
historia ya michuano hiyo tangia ianzishwe akiwa na magoli 104,mbele ya
mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi mwenye magoli 98.



Ili Atletico Madrid iweze kutinga fainali ya michuano hiyo itahitaji
miujiza ya Mungu kwa Klabu ya Madrid kuruhusu Magoli Manne au zaidi ili
ikate tiketi ya kucheza fainali.



Fainali ya Klabu Bingwa barani ulaya itachezwa mnamo tarehe 03/June mwaka huu kunako dimba la Cardiff,huko nchini Uingereza

Comments

Popular posts from this blog

je wajua,zifahamu mbinu mbalimbali za kumpata mwenzi bora

KILA mtu anapenda kuwa na mwenza mzuri, mwenye kumfaa katika maisha yake. Hata hivyo kwa bahati mbaya ni kwamba wengi wanashindwa kupata wenza wazuri. Ziko sababu nyingi lakini kubwa ni uwezo wa mtu wa kumtambua mwingine na kujua kama ni kweli anafaa au anafaa  kuendana nae au la.Wakati wa uchumba, wengi wa watu huonekana kutumiana kadi, zawadi na mambo mengine  mbalimbali yenye lengo la kuonyesha wanapendana. Aidha, wapo ambao wanashindwa kujua namna ya kutongoza; kwa ujumla kutongoza ni uwezo wa ushawishi kwamba unamwambia mwanamke unamuhitaji na kumpenda awe wako au wakati mwingine hata mwanamke anaweza kuanza. Ndio ukweli wenyewe Sio kweli kwamba kila mwanaume anajua kutongoza. Kuna wengine hata kumsimamisha mwanamke hawezi au anaogopa. Ndio unaweza kukuta mwanamume anajikanyaga namna ya kuongea. Wapo wengine wanafikiri njia sahihi ya kutongoza ni kuhonga aidha fedha au mali nk, lakini sicho hasa wanachotaka wanawake au wanaume katika mapenzi. Maneno ya ku...

Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi

Hii Ndiyo Tafsiri sahihi Ya Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi Moja ya kitu ambacho huwa hakina kipaumbele sana katika mahusiano ya kimapenzi,  kitu ambacho kinachoitwa zawadi. Lakini ukweli ni kwamba zawadi ina maana kubwa sana katika mahusiano ya kimapenzi zaidi hata udhaniavyo. Na Katika tafiti ambazo zimewahi fanywa ni kwamba, suala zima la utoaji zawadi katika mahusiano ya kimapenzi lilimekuwa likileta hisia zaidi katika upande mmoja. Yaani hapa nikiwa na maana ya kwamba jinsia ya kike ndiyo ambayo ipo katika kusubiri zawadi kutoka kwa jinsia ya kiume. Kutoka na suala hilo ndo maana watu wengi wamekuwa hawatilii maanani suala zima la zawadi. Lakini ukweli ni kwamba kila mtu anahusika kutoa zawadi. Huenda ukawa bado nakuacha njia panda huelewi ni zawadi gani ambayo itampendeza mpenzi wako. Wala usipate tabu afisa Mipango nipo kwa ajili yako. Ipo hivi ili kujua zawadi ambayo mwezi wako anapendezwa nayo,  Unachotakiwa kukifanya ni kwamba kwa kuwa ni mpen...

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...