Skip to main content

Cristiano Ronaldo Amazing Hat-Trick vs Atletico Madrid (All Goals) 2016/17





Mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid na Timu ya Taifa ya Ureno,
Cristiano Ronaldo ameendeleza ubabe wake kwa kupiga Hatrick nyingine ya
pili mfululizo usiku wa jana kunako dimba la Santiago Bernabeu wakati
timu yake ilipovaana na mahasimu wao Atletico Madrid kwenye mchezo wa
kwanza hatua ya nusu fainali, Klabu Bingwa barani Ulaya.



Real Madrid-Atletico Madrid 3-0, l'uragano Ronaldo spazza via Simeone

Cristiano Ronaldo akishangilia goli lake la pili jana usiku dhidi ya Atletico.



Ronaldo alianza makeke yake kunako dakika ya 10′ ya mchezo huo kwa
kupiga kichwa kizito kilichopelekea mlinda mlango wa Atletico Madrid
kushindwa kuhimili mpira huo na Mreno huyo kucheka na nyavu.



Mpaka mpira unaenda mapumziko Atletico walikuwa wameshatandikwa goli
moja,na kipindi cha pili mashambulizi yaliwaelemea zaidi Atletico kwani
kunako dakika ya 73,Ronaldo alipiga shuti la mbali lililomuelemea goli
kipa kabla ya goli la tatu ambalo alifunga kunako ya 86′ na kumaliza
hesabu ya magoli 3-0,Na ikiwa pia ni Hatrick ya pili ya mfululizo baada
ya ile aliyowapiga Bayern Munich.



Ronaldo kwa sasa anakuwa ndiyo mchezaji mwenye magoli mengi zaidi kwenye
historia ya michuano hiyo tangia ianzishwe akiwa na magoli 104,mbele ya
mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi mwenye magoli 98.



Ili Atletico Madrid iweze kutinga fainali ya michuano hiyo itahitaji
miujiza ya Mungu kwa Klabu ya Madrid kuruhusu Magoli Manne au zaidi ili
ikate tiketi ya kucheza fainali.



Fainali ya Klabu Bingwa barani ulaya itachezwa mnamo tarehe 03/June mwaka huu kunako dimba la Cardiff,huko nchini Uingereza

Comments

Popular posts from this blog

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta...