Skip to main content

Cristiano Ronaldo Amazing Hat-Trick vs Atletico Madrid (All Goals) 2016/17





Mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid na Timu ya Taifa ya Ureno,
Cristiano Ronaldo ameendeleza ubabe wake kwa kupiga Hatrick nyingine ya
pili mfululizo usiku wa jana kunako dimba la Santiago Bernabeu wakati
timu yake ilipovaana na mahasimu wao Atletico Madrid kwenye mchezo wa
kwanza hatua ya nusu fainali, Klabu Bingwa barani Ulaya.



Real Madrid-Atletico Madrid 3-0, l'uragano Ronaldo spazza via Simeone

Cristiano Ronaldo akishangilia goli lake la pili jana usiku dhidi ya Atletico.



Ronaldo alianza makeke yake kunako dakika ya 10′ ya mchezo huo kwa
kupiga kichwa kizito kilichopelekea mlinda mlango wa Atletico Madrid
kushindwa kuhimili mpira huo na Mreno huyo kucheka na nyavu.



Mpaka mpira unaenda mapumziko Atletico walikuwa wameshatandikwa goli
moja,na kipindi cha pili mashambulizi yaliwaelemea zaidi Atletico kwani
kunako dakika ya 73,Ronaldo alipiga shuti la mbali lililomuelemea goli
kipa kabla ya goli la tatu ambalo alifunga kunako ya 86′ na kumaliza
hesabu ya magoli 3-0,Na ikiwa pia ni Hatrick ya pili ya mfululizo baada
ya ile aliyowapiga Bayern Munich.



Ronaldo kwa sasa anakuwa ndiyo mchezaji mwenye magoli mengi zaidi kwenye
historia ya michuano hiyo tangia ianzishwe akiwa na magoli 104,mbele ya
mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi mwenye magoli 98.



Ili Atletico Madrid iweze kutinga fainali ya michuano hiyo itahitaji
miujiza ya Mungu kwa Klabu ya Madrid kuruhusu Magoli Manne au zaidi ili
ikate tiketi ya kucheza fainali.



Fainali ya Klabu Bingwa barani ulaya itachezwa mnamo tarehe 03/June mwaka huu kunako dimba la Cardiff,huko nchini Uingereza

Comments

Popular posts from this blog

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...

KILIMO CHA KISASA CHA MPUNGA

Utangulizi Mpunga ni zao la pili la chakula kwa umuhimu linalolimwa sehemu nyingi nchini Tanzania. Umuhimu wa zao hili umeongezeka kuanzia muongo uliopita kutokana na jamii za mijini na vijijini kupendelea zaidi kula wali na kupunguza ulaji wa vyakula vingine na kulifanya zao hili kuwa la chakula na biashara. Mvua ni chanzo kikuu cha maji kwenye kilimo cha mpunga. Viwango vya mahitaji ya maji katika kukua kwa mpunga hutofautiana miongoni mwa aina za mpunga. Ni kwa jinsi hii mpunga hupandwa katika mazingira mbalimbali kutegemea na mahitaji yake ya maji. Zipo aina tatu kuu za mazingira yanayolimwa mpunga kulingana na upatikanaji wa maji na hali ya mwinuko wa nchi. Mazingira haya ni kilimo cha mpunga wa mabondeni kinachotegemea mvua (72%), kilimo cha mpunga wa kwenye miinuko (20%) na kilimo cha mpunga cha umwagiliaji (8%). Kiasi cha mpunga kinachozalishwa nchini kimekuwa kikiongezeka mwaka hadi mwaka kutoka tani 41,000 mwaka 1970 hadi tani 811,500 mwaka 1998. Ongezeko hi...