Skip to main content

Cristiano Ronaldo Amazing Hat-Trick vs Atletico Madrid (All Goals) 2016/17





Mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid na Timu ya Taifa ya Ureno,
Cristiano Ronaldo ameendeleza ubabe wake kwa kupiga Hatrick nyingine ya
pili mfululizo usiku wa jana kunako dimba la Santiago Bernabeu wakati
timu yake ilipovaana na mahasimu wao Atletico Madrid kwenye mchezo wa
kwanza hatua ya nusu fainali, Klabu Bingwa barani Ulaya.



Real Madrid-Atletico Madrid 3-0, l'uragano Ronaldo spazza via Simeone

Cristiano Ronaldo akishangilia goli lake la pili jana usiku dhidi ya Atletico.



Ronaldo alianza makeke yake kunako dakika ya 10′ ya mchezo huo kwa
kupiga kichwa kizito kilichopelekea mlinda mlango wa Atletico Madrid
kushindwa kuhimili mpira huo na Mreno huyo kucheka na nyavu.



Mpaka mpira unaenda mapumziko Atletico walikuwa wameshatandikwa goli
moja,na kipindi cha pili mashambulizi yaliwaelemea zaidi Atletico kwani
kunako dakika ya 73,Ronaldo alipiga shuti la mbali lililomuelemea goli
kipa kabla ya goli la tatu ambalo alifunga kunako ya 86′ na kumaliza
hesabu ya magoli 3-0,Na ikiwa pia ni Hatrick ya pili ya mfululizo baada
ya ile aliyowapiga Bayern Munich.



Ronaldo kwa sasa anakuwa ndiyo mchezaji mwenye magoli mengi zaidi kwenye
historia ya michuano hiyo tangia ianzishwe akiwa na magoli 104,mbele ya
mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi mwenye magoli 98.



Ili Atletico Madrid iweze kutinga fainali ya michuano hiyo itahitaji
miujiza ya Mungu kwa Klabu ya Madrid kuruhusu Magoli Manne au zaidi ili
ikate tiketi ya kucheza fainali.



Fainali ya Klabu Bingwa barani ulaya itachezwa mnamo tarehe 03/June mwaka huu kunako dimba la Cardiff,huko nchini Uingereza

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta...

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as...

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...