Skip to main content

Wazazi wapewa onyo kuhusu mlo wa kuku wa kisasa

 Dar es Salaam. Wazazi wametakiwa kuwa makini na vyakula wanavyowapa wanafamilia hasa kuku wa kisasa kwani imebainika kuwa ina vichocheo vinavyosababisha watoto kupevuka wakiwa na umri mdogo.

Alisema baadhi ya vyakula husababisha saratani.

Akizungumza kwenye mafunzo kwa wanawake wa  Kanisa la KKKT Dayosisi ya Pwani jimbo la Magharibi leo, Daktari Dominista Kombe ambaye ni miongoni mwa madaktari Bingwa wa magonjwa ya saratani nchini, ambaye  amewataka wazazi kuhakikisha familia inakula mlo bora ulio na mboga za majani na matunda kwa wingi.

"Usile makapi,wengi wanapenda kukoboa mahindi na kula ugali wa sembe lakini dona ndiyo unga mzuri wenye virutubisho, lakini pia muwe na utaratibu wa kupima afya kwa ujumla hasa kwa watu wenye umri wa miaka 45 na kuendelea saratani inashambulia zaidi,"alisema Dk Kombe ambaye ni mstaafu wa hospitali ya Ocean Road (2016)

 Mkuu wa jimbo la Magharibi Mchungaji Jacob Mwangomola aliipongeza Idara ya wanawake kwa kuona umuhimu wa kuandaa mafunzo hayo, ambayo yanalenga kuhakikisha waumini wanaishi wakiwa wanatambua hali ya afya waliyonayo, huku wengine wakipata nafasi ya kubadili tabia zinazohatarisha afya zao kwa ujumla.

 “Tunahubiri injili ambayo ni afya ya kiroho na kimwili tumeweka kipaumbele huko, lakini kupima afya ni jambo jema pia kwa sababu kuna magonjwa kama haya ya saratani yanazidi kushika kasi, tunatakiwa kupimwa ili wataalam husika nao watoe mwongozo wa kitatibu," alisema Mchungaji Mwangomola.

Comments

Popular posts from this blog

je wajua,zifahamu mbinu mbalimbali za kumpata mwenzi bora

KILA mtu anapenda kuwa na mwenza mzuri, mwenye kumfaa katika maisha yake. Hata hivyo kwa bahati mbaya ni kwamba wengi wanashindwa kupata wenza wazuri. Ziko sababu nyingi lakini kubwa ni uwezo wa mtu wa kumtambua mwingine na kujua kama ni kweli anafaa au anafaa  kuendana nae au la.Wakati wa uchumba, wengi wa watu huonekana kutumiana kadi, zawadi na mambo mengine  mbalimbali yenye lengo la kuonyesha wanapendana. Aidha, wapo ambao wanashindwa kujua namna ya kutongoza; kwa ujumla kutongoza ni uwezo wa ushawishi kwamba unamwambia mwanamke unamuhitaji na kumpenda awe wako au wakati mwingine hata mwanamke anaweza kuanza. Ndio ukweli wenyewe Sio kweli kwamba kila mwanaume anajua kutongoza. Kuna wengine hata kumsimamisha mwanamke hawezi au anaogopa. Ndio unaweza kukuta mwanamume anajikanyaga namna ya kuongea. Wapo wengine wanafikiri njia sahihi ya kutongoza ni kuhonga aidha fedha au mali nk, lakini sicho hasa wanachotaka wanawake au wanaume katika mapenzi. Maneno ya ku...

Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi

Hii Ndiyo Tafsiri sahihi Ya Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi Moja ya kitu ambacho huwa hakina kipaumbele sana katika mahusiano ya kimapenzi,  kitu ambacho kinachoitwa zawadi. Lakini ukweli ni kwamba zawadi ina maana kubwa sana katika mahusiano ya kimapenzi zaidi hata udhaniavyo. Na Katika tafiti ambazo zimewahi fanywa ni kwamba, suala zima la utoaji zawadi katika mahusiano ya kimapenzi lilimekuwa likileta hisia zaidi katika upande mmoja. Yaani hapa nikiwa na maana ya kwamba jinsia ya kike ndiyo ambayo ipo katika kusubiri zawadi kutoka kwa jinsia ya kiume. Kutoka na suala hilo ndo maana watu wengi wamekuwa hawatilii maanani suala zima la zawadi. Lakini ukweli ni kwamba kila mtu anahusika kutoa zawadi. Huenda ukawa bado nakuacha njia panda huelewi ni zawadi gani ambayo itampendeza mpenzi wako. Wala usipate tabu afisa Mipango nipo kwa ajili yako. Ipo hivi ili kujua zawadi ambayo mwezi wako anapendezwa nayo,  Unachotakiwa kukifanya ni kwamba kwa kuwa ni mpen...

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...