Skip to main content

Wazazi wapewa onyo kuhusu mlo wa kuku wa kisasa

 Dar es Salaam. Wazazi wametakiwa kuwa makini na vyakula wanavyowapa wanafamilia hasa kuku wa kisasa kwani imebainika kuwa ina vichocheo vinavyosababisha watoto kupevuka wakiwa na umri mdogo.

Alisema baadhi ya vyakula husababisha saratani.

Akizungumza kwenye mafunzo kwa wanawake wa  Kanisa la KKKT Dayosisi ya Pwani jimbo la Magharibi leo, Daktari Dominista Kombe ambaye ni miongoni mwa madaktari Bingwa wa magonjwa ya saratani nchini, ambaye  amewataka wazazi kuhakikisha familia inakula mlo bora ulio na mboga za majani na matunda kwa wingi.

"Usile makapi,wengi wanapenda kukoboa mahindi na kula ugali wa sembe lakini dona ndiyo unga mzuri wenye virutubisho, lakini pia muwe na utaratibu wa kupima afya kwa ujumla hasa kwa watu wenye umri wa miaka 45 na kuendelea saratani inashambulia zaidi,"alisema Dk Kombe ambaye ni mstaafu wa hospitali ya Ocean Road (2016)

 Mkuu wa jimbo la Magharibi Mchungaji Jacob Mwangomola aliipongeza Idara ya wanawake kwa kuona umuhimu wa kuandaa mafunzo hayo, ambayo yanalenga kuhakikisha waumini wanaishi wakiwa wanatambua hali ya afya waliyonayo, huku wengine wakipata nafasi ya kubadili tabia zinazohatarisha afya zao kwa ujumla.

 “Tunahubiri injili ambayo ni afya ya kiroho na kimwili tumeweka kipaumbele huko, lakini kupima afya ni jambo jema pia kwa sababu kuna magonjwa kama haya ya saratani yanazidi kushika kasi, tunatakiwa kupimwa ili wataalam husika nao watoe mwongozo wa kitatibu," alisema Mchungaji Mwangomola.

Comments

Popular posts from this blog

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...

KILIMO CHA KISASA CHA MPUNGA

Utangulizi Mpunga ni zao la pili la chakula kwa umuhimu linalolimwa sehemu nyingi nchini Tanzania. Umuhimu wa zao hili umeongezeka kuanzia muongo uliopita kutokana na jamii za mijini na vijijini kupendelea zaidi kula wali na kupunguza ulaji wa vyakula vingine na kulifanya zao hili kuwa la chakula na biashara. Mvua ni chanzo kikuu cha maji kwenye kilimo cha mpunga. Viwango vya mahitaji ya maji katika kukua kwa mpunga hutofautiana miongoni mwa aina za mpunga. Ni kwa jinsi hii mpunga hupandwa katika mazingira mbalimbali kutegemea na mahitaji yake ya maji. Zipo aina tatu kuu za mazingira yanayolimwa mpunga kulingana na upatikanaji wa maji na hali ya mwinuko wa nchi. Mazingira haya ni kilimo cha mpunga wa mabondeni kinachotegemea mvua (72%), kilimo cha mpunga wa kwenye miinuko (20%) na kilimo cha mpunga cha umwagiliaji (8%). Kiasi cha mpunga kinachozalishwa nchini kimekuwa kikiongezeka mwaka hadi mwaka kutoka tani 41,000 mwaka 1970 hadi tani 811,500 mwaka 1998. Ongezeko hi...