Skip to main content

Wazazi wapewa onyo kuhusu mlo wa kuku wa kisasa

 Dar es Salaam. Wazazi wametakiwa kuwa makini na vyakula wanavyowapa wanafamilia hasa kuku wa kisasa kwani imebainika kuwa ina vichocheo vinavyosababisha watoto kupevuka wakiwa na umri mdogo.

Alisema baadhi ya vyakula husababisha saratani.

Akizungumza kwenye mafunzo kwa wanawake wa  Kanisa la KKKT Dayosisi ya Pwani jimbo la Magharibi leo, Daktari Dominista Kombe ambaye ni miongoni mwa madaktari Bingwa wa magonjwa ya saratani nchini, ambaye  amewataka wazazi kuhakikisha familia inakula mlo bora ulio na mboga za majani na matunda kwa wingi.

"Usile makapi,wengi wanapenda kukoboa mahindi na kula ugali wa sembe lakini dona ndiyo unga mzuri wenye virutubisho, lakini pia muwe na utaratibu wa kupima afya kwa ujumla hasa kwa watu wenye umri wa miaka 45 na kuendelea saratani inashambulia zaidi,"alisema Dk Kombe ambaye ni mstaafu wa hospitali ya Ocean Road (2016)

 Mkuu wa jimbo la Magharibi Mchungaji Jacob Mwangomola aliipongeza Idara ya wanawake kwa kuona umuhimu wa kuandaa mafunzo hayo, ambayo yanalenga kuhakikisha waumini wanaishi wakiwa wanatambua hali ya afya waliyonayo, huku wengine wakipata nafasi ya kubadili tabia zinazohatarisha afya zao kwa ujumla.

 “Tunahubiri injili ambayo ni afya ya kiroho na kimwili tumeweka kipaumbele huko, lakini kupima afya ni jambo jema pia kwa sababu kuna magonjwa kama haya ya saratani yanazidi kushika kasi, tunatakiwa kupimwa ili wataalam husika nao watoe mwongozo wa kitatibu," alisema Mchungaji Mwangomola.

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyin