Skip to main content

Ushindi wa Yanga vs Prisons presha kwa Simba

Mabingwa watetezi wa tajin la VPL Young Africans wamerejea kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kupata ushinsi wa magoli 2-0 dhidi ya Tanzania Prisons mchezo uliopigwa uwanja wa taifa.

Yanga imefikisha jumla ya pointi 59 sawa na watani zao Simba lakini Yanga wana wastani mzuri wa magoli ukilinganisha na Simba na ndio kitu kilichowaweka kwenye nafasi ya kwanza ya msimamo wa ligi. Yanga wana wastaani wa magoli 41 wakati Simba wao wakiwa na wastani wa magoli 30.

Ki8kosi cha Yanga bado kina faida ya mechi moja mkononi, hadi sasa wamecheza mechi 26 mechi moja nyuma ya Simba ambao tayari wameshacheza mechi 27 hadi sasa wakibakiza michezo mitatu tu kumaliza msimu wa ligi 2016-2017.

Amis Tambwe alianza kufunga goli la kwanza dakika ya 71 kipindi cha pili shambulizi likianzia kwa Simon Msuva ambaye alitoa pande kwa Obrey Chirwa kisha Chirwa akatoa pasi kwa Juma Abdul ambaye akatia krosi ya juu ikamkuta Tambwe aliyejitwisha na kuifungia Yanga bao la kwanza.

Dakika nne baadaye Tanzania Prisons wakaruhusu bao la pili lililofungwa na Chirwa dakika ya 75 baada ya Niyonzima kumuwekea pasi Joffrey Mwashiuya ambaye alipiga krosi ya juu ikapigwa kichwa na Tambwe na kuurudisha mpira kwenye eneo la 18 kisha Chirwa akafunga kwa kichwa.

Mabadiliko yaliyofanywa na kocha wa Yanga George Lwandamina kwa kuwaingiza Haruna Niyonzima, Juma Abdul na baadae Matheo Anthony yalichangia kuipa Yanga nguvu na kupata magoli mawili ya haraka.

Yanga imefunga magoli yote mawili kutokana na krosi, goli la kwanza limefungwa baada ya krosi ya Juma Abdul wakati bao la pili lilitokana na krosi ya Geoffrey Mwahsiuya.

Matukio katika namba
10 – Obrey Chirwa na Amis Tambwe kila mmoja amefikisha magoli 10 baada ya kila mmoja kufunga goli moja dhidi ya Tanzania Prisons.

6 – Magoli ambayo Yanga wameifunga Prisons katika msimu huu. (VPL) 06/11/2016 Tanzania Prisons 0-1 Yanga, 06/05/2017 Yanga 2-0 Tanzania Prisons na (Azam Sports Federation Cup) 22/04/2017 Yanga 3-0 Tanzania Prisons.

3 – Mechi ambazo Yanga na Prisons wamekutana katika msimu huu (2016-2017) mechi mbili zikiwa ni za ligi na moja ya mchezo wa robo fainali ya Azam Sports Federation Cup. Mechi zote Yanga wameshinda

Comments

Popular posts from this blog

je wajua,zifahamu mbinu mbalimbali za kumpata mwenzi bora

KILA mtu anapenda kuwa na mwenza mzuri, mwenye kumfaa katika maisha yake. Hata hivyo kwa bahati mbaya ni kwamba wengi wanashindwa kupata wenza wazuri. Ziko sababu nyingi lakini kubwa ni uwezo wa mtu wa kumtambua mwingine na kujua kama ni kweli anafaa au anafaa  kuendana nae au la.Wakati wa uchumba, wengi wa watu huonekana kutumiana kadi, zawadi na mambo mengine  mbalimbali yenye lengo la kuonyesha wanapendana. Aidha, wapo ambao wanashindwa kujua namna ya kutongoza; kwa ujumla kutongoza ni uwezo wa ushawishi kwamba unamwambia mwanamke unamuhitaji na kumpenda awe wako au wakati mwingine hata mwanamke anaweza kuanza. Ndio ukweli wenyewe Sio kweli kwamba kila mwanaume anajua kutongoza. Kuna wengine hata kumsimamisha mwanamke hawezi au anaogopa. Ndio unaweza kukuta mwanamume anajikanyaga namna ya kuongea. Wapo wengine wanafikiri njia sahihi ya kutongoza ni kuhonga aidha fedha au mali nk, lakini sicho hasa wanachotaka wanawake au wanaume katika mapenzi. Maneno ya ku...

Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi

Hii Ndiyo Tafsiri sahihi Ya Zawadi Katika Mahusiano Ya Kimapenzi Moja ya kitu ambacho huwa hakina kipaumbele sana katika mahusiano ya kimapenzi,  kitu ambacho kinachoitwa zawadi. Lakini ukweli ni kwamba zawadi ina maana kubwa sana katika mahusiano ya kimapenzi zaidi hata udhaniavyo. Na Katika tafiti ambazo zimewahi fanywa ni kwamba, suala zima la utoaji zawadi katika mahusiano ya kimapenzi lilimekuwa likileta hisia zaidi katika upande mmoja. Yaani hapa nikiwa na maana ya kwamba jinsia ya kike ndiyo ambayo ipo katika kusubiri zawadi kutoka kwa jinsia ya kiume. Kutoka na suala hilo ndo maana watu wengi wamekuwa hawatilii maanani suala zima la zawadi. Lakini ukweli ni kwamba kila mtu anahusika kutoa zawadi. Huenda ukawa bado nakuacha njia panda huelewi ni zawadi gani ambayo itampendeza mpenzi wako. Wala usipate tabu afisa Mipango nipo kwa ajili yako. Ipo hivi ili kujua zawadi ambayo mwezi wako anapendezwa nayo,  Unachotakiwa kukifanya ni kwamba kwa kuwa ni mpen...

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...