Skip to main content

Ushindi wa Yanga vs Prisons presha kwa Simba

Mabingwa watetezi wa tajin la VPL Young Africans wamerejea kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kupata ushinsi wa magoli 2-0 dhidi ya Tanzania Prisons mchezo uliopigwa uwanja wa taifa.

Yanga imefikisha jumla ya pointi 59 sawa na watani zao Simba lakini Yanga wana wastani mzuri wa magoli ukilinganisha na Simba na ndio kitu kilichowaweka kwenye nafasi ya kwanza ya msimamo wa ligi. Yanga wana wastaani wa magoli 41 wakati Simba wao wakiwa na wastani wa magoli 30.

Ki8kosi cha Yanga bado kina faida ya mechi moja mkononi, hadi sasa wamecheza mechi 26 mechi moja nyuma ya Simba ambao tayari wameshacheza mechi 27 hadi sasa wakibakiza michezo mitatu tu kumaliza msimu wa ligi 2016-2017.

Amis Tambwe alianza kufunga goli la kwanza dakika ya 71 kipindi cha pili shambulizi likianzia kwa Simon Msuva ambaye alitoa pande kwa Obrey Chirwa kisha Chirwa akatoa pasi kwa Juma Abdul ambaye akatia krosi ya juu ikamkuta Tambwe aliyejitwisha na kuifungia Yanga bao la kwanza.

Dakika nne baadaye Tanzania Prisons wakaruhusu bao la pili lililofungwa na Chirwa dakika ya 75 baada ya Niyonzima kumuwekea pasi Joffrey Mwashiuya ambaye alipiga krosi ya juu ikapigwa kichwa na Tambwe na kuurudisha mpira kwenye eneo la 18 kisha Chirwa akafunga kwa kichwa.

Mabadiliko yaliyofanywa na kocha wa Yanga George Lwandamina kwa kuwaingiza Haruna Niyonzima, Juma Abdul na baadae Matheo Anthony yalichangia kuipa Yanga nguvu na kupata magoli mawili ya haraka.

Yanga imefunga magoli yote mawili kutokana na krosi, goli la kwanza limefungwa baada ya krosi ya Juma Abdul wakati bao la pili lilitokana na krosi ya Geoffrey Mwahsiuya.

Matukio katika namba
10 – Obrey Chirwa na Amis Tambwe kila mmoja amefikisha magoli 10 baada ya kila mmoja kufunga goli moja dhidi ya Tanzania Prisons.

6 – Magoli ambayo Yanga wameifunga Prisons katika msimu huu. (VPL) 06/11/2016 Tanzania Prisons 0-1 Yanga, 06/05/2017 Yanga 2-0 Tanzania Prisons na (Azam Sports Federation Cup) 22/04/2017 Yanga 3-0 Tanzania Prisons.

3 – Mechi ambazo Yanga na Prisons wamekutana katika msimu huu (2016-2017) mechi mbili zikiwa ni za ligi na moja ya mchezo wa robo fainali ya Azam Sports Federation Cup. Mechi zote Yanga wameshinda

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyin