Skip to main content

Ushindi wa Yanga vs Prisons presha kwa Simba

Mabingwa watetezi wa tajin la VPL Young Africans wamerejea kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kupata ushinsi wa magoli 2-0 dhidi ya Tanzania Prisons mchezo uliopigwa uwanja wa taifa.

Yanga imefikisha jumla ya pointi 59 sawa na watani zao Simba lakini Yanga wana wastani mzuri wa magoli ukilinganisha na Simba na ndio kitu kilichowaweka kwenye nafasi ya kwanza ya msimamo wa ligi. Yanga wana wastaani wa magoli 41 wakati Simba wao wakiwa na wastani wa magoli 30.

Ki8kosi cha Yanga bado kina faida ya mechi moja mkononi, hadi sasa wamecheza mechi 26 mechi moja nyuma ya Simba ambao tayari wameshacheza mechi 27 hadi sasa wakibakiza michezo mitatu tu kumaliza msimu wa ligi 2016-2017.

Amis Tambwe alianza kufunga goli la kwanza dakika ya 71 kipindi cha pili shambulizi likianzia kwa Simon Msuva ambaye alitoa pande kwa Obrey Chirwa kisha Chirwa akatoa pasi kwa Juma Abdul ambaye akatia krosi ya juu ikamkuta Tambwe aliyejitwisha na kuifungia Yanga bao la kwanza.

Dakika nne baadaye Tanzania Prisons wakaruhusu bao la pili lililofungwa na Chirwa dakika ya 75 baada ya Niyonzima kumuwekea pasi Joffrey Mwashiuya ambaye alipiga krosi ya juu ikapigwa kichwa na Tambwe na kuurudisha mpira kwenye eneo la 18 kisha Chirwa akafunga kwa kichwa.

Mabadiliko yaliyofanywa na kocha wa Yanga George Lwandamina kwa kuwaingiza Haruna Niyonzima, Juma Abdul na baadae Matheo Anthony yalichangia kuipa Yanga nguvu na kupata magoli mawili ya haraka.

Yanga imefunga magoli yote mawili kutokana na krosi, goli la kwanza limefungwa baada ya krosi ya Juma Abdul wakati bao la pili lilitokana na krosi ya Geoffrey Mwahsiuya.

Matukio katika namba
10 – Obrey Chirwa na Amis Tambwe kila mmoja amefikisha magoli 10 baada ya kila mmoja kufunga goli moja dhidi ya Tanzania Prisons.

6 – Magoli ambayo Yanga wameifunga Prisons katika msimu huu. (VPL) 06/11/2016 Tanzania Prisons 0-1 Yanga, 06/05/2017 Yanga 2-0 Tanzania Prisons na (Azam Sports Federation Cup) 22/04/2017 Yanga 3-0 Tanzania Prisons.

3 – Mechi ambazo Yanga na Prisons wamekutana katika msimu huu (2016-2017) mechi mbili zikiwa ni za ligi na moja ya mchezo wa robo fainali ya Azam Sports Federation Cup. Mechi zote Yanga wameshinda

Comments

Popular posts from this blog

KILIMO BORA CHA MIGOMBA

  Na Daniel Mbega,   MaendeleoVijijini KWA miaka mingi ndizi ndilo zao kuu la chakula mkoani Kagera, na sasa limekuwa zao la biashara kwa baadhi ya wilaya kama Karagwe na Muleba. Ndizi zinasafirishwa kwa wingi kwenda mikoa mingine ndani na nje ya Kanda ya Ziwa na zinaonekana kupendwa na walaji wengi, hasa ‘Ndizi Bukoba’. Ndizi zinatokana na migomba. MaendeleoVijijini   inafahamu kwamba, japokuwa kuna mazao mengine yanayolimwa Kagera kama kahawa, mahindi, maharage, mikunde, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, njugu mawe, karanga, nyanya, machungwa, mapera na mananasi , lakini migomba ndilo zao linaloongoza kwa chakula. Mbali ya Kagera, migomba hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Morogoro, Tanga, Mbeya, Kigoma na Mara. Taarifa ambazo MaendeleoVijijini inazo zinaonyesha kwamba, wastani wa uzalishaji wa ndizi nchini Tanzania ni tani 665,000 kwa mwaka. Matumizi:   Matumizi makuu ya ndizi ni chakula – wenyeji wa Kagera hutumia...

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...

KILIMO CHA KISASA CHA MPUNGA

Utangulizi Mpunga ni zao la pili la chakula kwa umuhimu linalolimwa sehemu nyingi nchini Tanzania. Umuhimu wa zao hili umeongezeka kuanzia muongo uliopita kutokana na jamii za mijini na vijijini kupendelea zaidi kula wali na kupunguza ulaji wa vyakula vingine na kulifanya zao hili kuwa la chakula na biashara. Mvua ni chanzo kikuu cha maji kwenye kilimo cha mpunga. Viwango vya mahitaji ya maji katika kukua kwa mpunga hutofautiana miongoni mwa aina za mpunga. Ni kwa jinsi hii mpunga hupandwa katika mazingira mbalimbali kutegemea na mahitaji yake ya maji. Zipo aina tatu kuu za mazingira yanayolimwa mpunga kulingana na upatikanaji wa maji na hali ya mwinuko wa nchi. Mazingira haya ni kilimo cha mpunga wa mabondeni kinachotegemea mvua (72%), kilimo cha mpunga wa kwenye miinuko (20%) na kilimo cha mpunga cha umwagiliaji (8%). Kiasi cha mpunga kinachozalishwa nchini kimekuwa kikiongezeka mwaka hadi mwaka kutoka tani 41,000 mwaka 1970 hadi tani 811,500 mwaka 1998. Ongezeko hi...