Skip to main content

Yanga yajisafisha kuhusu taarifa zinazoendelea kwenye mitandao

Klabu ya Yanga imesafisha hali ya hewa kutokana na taarifa zinazovumishwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kuachwa kwa baadhi ya wachezaji itakapofika mwishoni mwa msimu huu kutokana na matatizo ya kiuchumi kwenye klabu hiyo.

Taarifa iliyotolewa na Katibu mkuu Yanga, Charles Boniface Mkwasa imeeleza kuwa, hakuna ukweli wowote wa taarifa za kuachwa kwa wachezaji, na huenda zina malengo ya kuanza kuwavuruga katika kipindi hiki cha kuelekea mwishoni mwa msimu.

“Taarifa hizo ni za uongo na uzushi mkubwa . Uongozi upo bega kwa bega na wachezaji wote 27 na benchi lao la ufundi. Hatujakaa kulijadili hilo wala kulifikiria bali tupo makini kutetea ubingwa wetu wa ligi kuu.”

“Mwenye maamuzi ya mwisho juu ya huduma ya wachezaji klabuni kwetu ni kocha mkuu Mr George Lwandamina na timu yake sio kiongozi mwingine yoyote na kocha huyo hajatoa taarifa yoyote ya kumwacha mchezaji gani au yupi kumuongezea mkataba zaidi ya kila siku kuukazania uongozi kuboresha masilahi yao kwa sababu kama kocha mkuu anajivunia na kujali kazi ya vijana wake.” Imeeleza taarifa ya Katibu mkuu wa Klabu ya Yanga,Ndg Mkwasa.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa, wachezaji wote ni muhimu na uongozi wa Yanga unajivunia kwa moyo wao thabiti kuitumikia klabu. Hivyo wamewaomba wachezaji kuwapuuza watoa habari feki za klabu, na badala yake waendelee kucheza kwa bidii.

Klabu ya Yanga ipo kambini mkoani Geita ambako jana iliibuka na ushindi wa goli 5-0 kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Buseresere,Na hii ni salamu tosha kwa maafande wa Tanzania Prisons ambao watavaana nao Jumamosi ya wikiendi hii kunako dimba la taifa.

Timu hiyo, ilipata ushindi huo katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Waja uliopo Mkoani Geita. @muungwana.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta...

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as...

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...