Skip to main content

Nyuma ya Pazia kifo cha Mume wa Zari

 KAMPALA: Kifo cha aliyekuwa mume wa staa wa Uganda na Afrika Mashariki, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, Tycoon Ivan Semwanga ‘The Don’, raia wa Uganda, mwenye maskani yake Johannesburg na Pretoria, Afrika Kusini, kimeibua simulizi nzito nyuma ya pazia.

Kwa mujibu wa chanzo cha ndani ya familia ya Ivan iliyopo Muyenga jijini Kampala, kilichokaririwa na mitandao ya kuaminika nchini Uganda, katika siku za mwisho za maisha yake kabla ya kuripotiwa kupatwa na ugonjwa wa shambulio la moyo ambao kitaalam huitwa Coronary Artery Disease (CAD). Ilifahamika kuwa, ugonjwa huo ndiyo uliomsababishia kifo usiku wa kuamkia juzi.

Habari zilieleza kuwa, Ivan alionekana kwa mara ya mwisho kwenye Pati ya Blankets and Wine iliyofanyika huko Kampala, Uganda wiki mbili zilizopita. Ilielezwa kuwa, rais huyo wa Kundi la Rich Gang, mwenye umri wa miaka 39, alionekana aliyedhoofu na asiyekuwa na furaha kama kawaida yake huku akinywa soda na kula samaki, tofauti na alivyozoeleka kuwa ni mtu wa kupiga vinywaji vikali, tena vya bei mbaya. “Nyuma ya hali yake kiafya alionekana dhahiri mwenye matatizo yaliyosababisha hata kula yake kuwa ya kusuasua na kusababisha hali kuwa mbaya zaidi,” kilikaririwa chanzo hicho.

CHANZO CHA UGONJWA

Chanzo hicho kilidai kuwa, chanzo cha Ivan kupatwa na ugonjwa huo ni pale alipotokea Sauzi na kwenda kuangalia moja ya mali zake (mashamba makubwa) zilizopo Kampala na kukuta kuna watu wamebadilisha umiliki bila yeye kujua. Ilisemekana kuwa, kuna wakazi waliotengeneza nyaraka na hati za kumiliki ardhi ya jamaa huyo ambayo ilionesha walikuwa wamiliki wapya ilihali ni mali ya jamaa huyo.

Wakati watu hao wakifanya hivyo, Ivan hakujua kilichokuwa kikiendelea. Ilielezwa kwamba, ishu hiyo ilimsababishia Ivan mshtuko wa moyo na maumivu makali ya kichwa ambayo pia yaliathiri utendaji wake wa kazi wa kila siku.

Mbali na hilo, pia, kuliibuka taarifa za kuuzwa kwa nyumba yake na watu wasiojulikana ambapo alitumia nguvu kubwa kukanusha taarifa hizo na kueleza kuwa kwa utajiri alionao hawezi kuuza nyumba yake ya kifahari iliyopo Munyonyo, Kampala.

“Mwishowe, alipoona hali yake kiafya inakuwa mbaya kutokana na mshtuko uliotokana na mambo hayo, Ivan alichukua ndege na kwenda Afrika Kusini kisha kuripoti mwenyewe katika Hospitali ya Steve Biko Academy iliyopo Pretoria. “Vipimo vilionesha kuwa alipatwa na mshtuko wa moyo ambao ulisababishwa na kuganda kwa damu kwenye mishipa,” alisema sosi huyo wa jijini Kampala. Mwishoni mwa wiki iliyopita, baba huyo wa watoto watatu aliozaa na Zari alielezwa kuwa hali yake ilizidi kuwa mbaya zaidi hivyo kufanyiwa operesheni kubwa ya kichwa.

ZARI ATHIBITISHA

Kupitia ukurasa wake Mtandao wa Kijamii wa Instagram, Zari alithibitisha kifo cha mumewe ambapo aliandika
waraka wa simanzi: “Mungu huwapenda wale ambao ni maalum kwake ndivyo ulivyokuwa, umewagusa na kuwasaidia maelfu, ulifanya mengi ya kushangaza na nakumbuka maneno yako ‘maisha ni mafupi mno, acha tuishi kwa ukamilifu’. Hii ni saa ya giza, sasa naelewa kwa nini ulikuwa ukisema maneno hayo kwangu. “Kwa wanao, umekuwa shujaa -aina fulani ya superman. Mtu yeyote ambaye amewahi kuwa karibu yako anajua wewe ni mtu wa aina gani, anajua ucheshi wako.

Watu watakumisi na kukumbuka sana kwa namna nyingi…Ulikuwa IVAN DON.

Baadhi ya mastaa wa Uganda walieleza ni namna gani walivyoshtushwa na kifo cha Ivan. Bebe Cool –Natoa rambirambi zangu za dhati kwake na familia yake. RIP kaka IVAN. Jose Chameleone -Mungu anaumba na kuchukua kilicho chake! Mungu akurehemu rafiki yangu na kuimarisha familia yako na sisi rafiki zako. Pumzika kwa amani Ivan. Ed Cheune –Ulieneza furaha miaka yote ulipokuwa nasi wote, sasa ni zamu ya Mungu kukupa furaha yote katika kurudi kwako kwake.

Pumzika kwa amani ndugu yangu mpendwa Ivan Semwanga. Baadhi ya mastaa wa Kibongo walioandika mitandaoni kumlilia Ivan ni pamoja na Wema Isaac Sepetu, Emmanuel Mbasha, Ali Kiba, Ester Kiama, Shilole na wengine wengi kutokana na ukaribu wake na wao. Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, bado utaratibu wa mazishi ulikuwa haujawekwa wazi. Ivan alipata umaarufu Afrika Mashariki kutokana na biashara zake kubwa ikiwemo umiliki wa vyuo mbalimbali nchini Afrika Kusini huku akisifika kwa kusaidia shughuli za kijamii nchini Uganda.

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as

Vyakula 4 vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake

Wanawake wengi wanaokaribia ukomo wa hedhi au waliokoma hedhi tayari(menopause) hukosa hamu ya tendo la ndoa. Wataalamu wa afya wameshauri vyakula vinavyoweza kuwapa wanawake hamu  ya tendo la ndoa. Mtaalamu wa Saikolojia wa Uingereza, Cassie Bjork, anasema badala ya kutumia dawa (Viagra) vya kuongeza hamu ya tendo la ndoa kuna vyakula maalum. Spinachi Wataalamu hao wanasema mboga ya majani aina ya spinachi ina wingi wa madini ya magnesium ambayo husaidia kusambaza damu kwenye mirija. Damu inaposambaa vyema mwilini hata hamu ya tendo la ndoa huongezeka. Bjork anasema kula kwa wingi mboga hizo kunamsaidia mwanamke hata kufikia kilele. Chai ya Kijani (Green tea) Chai ya kijani ina kompaundi iitwayo catechins. Hii inaelezwa kuwa inasaidia kuyeyusha mafuta mwilini. Lakini pia inalisaidia ini  kuchuja sumu na kuisaidia mishipa ya damu kufanya kazi vizuri. Damu ikitembea vyema mwilini, ni rahisi kwa mwanamke kujisikia hamu ya tendo.  Mafuta ya samaki  Zipo aina nyin