Skip to main content

Umesikia alichokisema Alikiba kuhusu Niyonzima?

Mkali wa Bongofleva Ali Kiba ni shabiki mkubwa Yanga na huwa hajifichi katika hilo huku mara kahaa akionekana uwanjani kuisapoti timu yake inapokuwa inacheza mechi mbalimbali.

Mbali na ushabiki wake wa Yanga, Ali Kiba na kiungo Haruna Niyonzima ni washkaji sana. Sasa Niyonzima ameondoka Yanga na haijafahamika hadi sasa anaelekea wapi ingawa anahusishwa kujiunga na Simba.

Kiba anazungumzia anavyojisikia baada ya uongozi wa Yanga kutangaza rasmi kwamba Niyonzima hata kuwa miongoni mwa wachezaji wao kuanzia msimu ujao.

“Nimejisikia vibaya kwa sababu mimi ni shabiki wa Yanga namkubali Niyonzima, lakini mpira ni kazi yake unapokuwa unatumikia sehemu kwa muda mrefu inafika kipindi unataka kwenda sehemu nyingine.”

“Kwanza ni historia nzuri kwake kwenye mpira kwamba amecheza klabu fulani na fulani, anatajwa kwenda Simba, ni klabu kubwa vilevile.”

“Nitaendelea kum-support kama mshkaji wangu lakini mimi ni shabiki wa Yanga na sija-mind yeye kutoka Yanga kwa sababu ni moja ya mafanikio kwake ameangalia maslahi na yeye ni mchezaji mpira.”

“Mchezaji mpira anafanana na sisi wanamuziki, tunaangalia panapokuwa na maslahi. Hata leo promota akiniambia ana kiasi hiki halafu mwingine akanipigia simu akaniambia ana zaidi nakwenda kwingine.”

“Vilevile sidhani kama amefanya maamuzi mabaya japokuwa mimi ni mwana Yanga na nilitamani aendelee kubaki Yanga ila ana uhuru.”

Niyonzima amewahi kuonekana mara kadhaa jukwaani kwenye show za Ali Kiba na wawili hao wamekuwa marafiki kwa muda mrefu sana.

Comments

Popular posts from this blog

Njia 3 za kuagana na maumivu ya jino haraka

Kwa kawaida hushauriwa kuwaona wataalam wa meno pale unapopata maumivu makali ya meno, lakini zipo njia za asili kadhaa ambazo huweza kupunguza ukali wa maumivu ya meno. Kama wengi wetu tunavyofahamu mara nyingi maumivu ya meno hutokea zaidi nyakati za usiku ambapo unakuwa huwezi kabisa kufika hospitali kwa ajili ya kuwaona wataalam wa meno au kung'oa kabisa na ndio maana leo nimeona nikufundishe mbinu hizi ya kupunguza maumivu hayo wakati ukisubiri kukuche ili ufike hospitali. 1. Kwanza kabisa unaweza kutumia kitunguu swaumu Hiki ni kiungo ambacho huweza kufananishwa na antibiotic kutokana na uwezo wake wa kuua vijidudu haraka. Unachopaswa kufanya ni kusaga kitunguu swaumu chako kisha changanya na chumvi kiasi halafu tumia mchanganyiko huo kwa kuweka moja kwa moja kwenye jino lenye maumivu au tatizo. 2. Pia unaweza kutumia kitunguu maji Hiki utakitafuna taratibu hususani  kwenye eneo lenye jino ambalo linasababisha maumivu kwa wakati huo, lakini pia kama kuta...

Faida 27 Za Kiafya Zipatikanazo Kwa Kutumia Asali Na Mdalasini

MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza kuongezwa maradufu kama itachanganywa na mdalasini wa kawaida. Uchunguzi wa kina ufanywao kwa wiki na jarida la World News wa Tiba, wataalamu wa madawa yatokanayo na mimea pamoja na kijarida cha afya na lishe, imeonekana kwamba kuna dazani nyingi za umuhimu wa asali na mdalasini pamoja na michanganyiko {dawa} ya kusisimua iletayo afya bora. Kama ifuatayo: 1. Ugonjwa wa Viungo/Maumivu na Uvimbe {ARTHRITIS}. Wataalamu wa lishe wanapendekeza kuchukua kwa kutumia mchanganyiko wa sehemu moja ya asali pamoja na sehemu mbli za maji vuguvugu na kijiko kimoja {cha chai} chenye mdalasini - na kuchua sehemu zilizoathirika. Nafuu hupatikana katika muda wa dakika moja. Vinginevyo tengeneza chai-kikombe kimoja chenye maji moto, weka vijiko vya chakula -viwili vya as...

Jinsi Ya Kuondokana na Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra. Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani maana ya kifungo hicho. ''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo. Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya. Mara kadhaa maisha yetu yame...