Skip to main content

Posts

Easy Way to Download Video on YouTube

Recent posts

lama pozz star new song (nielewe)

Roma Afunguka sababu ya kutozungumzia Kutekwa kwake

Roma Mkatoliki amefunguka na kuweka wazi sababu kubwa zilizomfanya kutokusema nini kilichopelekea yeye kutekwa na nini kilikuwa kinaendelea wakati akiwa chimbo na kudai aliamua kutumia busara ya kutokusema ili mwisho siku aendelee na kazi ya muziki. Roma Mkatoliki amesema hayo kupitia kipindi cha Friday Night Live (FNL) na kusema alitambua kuwa anaweza kuwakwaza baadhi ya watu kwa kutokusema na kuweka wazi lakini alifanya maamuzi hayo kwa lengo la kulinda sanaa yake na maisha yake kiujumla. "Mimi najua nini kilipelekea wale jamaa kututeka ni zaidi ya muziki japo chanzo ni muziki ndiyo maana walikuja kututeka tukiwa studio na si kanisani, wala nyumbani unajua wananchi tayari walikuwa na video kichwani, wakijua Roma anakuja kuongea hiki na kile tunamaliza pale halafu usiku mwema, lile tukio lilikuwa linahitaji busara ili maisha yaweze kuendelea,labda ningesema ukweli pengine ungekuwa mwisho wa Roma kwenye muziki, mashabiki wangeshangilia lakini wadau mbalimbali mc
Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars leo July 7 2017 imefanikiwa kuingia kwenye headlines baada ya kupata ushindi katika game ya michuano ya COSAFA ya kutafuta mshindi wa tatu iliyochezwa Afrika Kusini. Taifa Stars game ya kutafuta mshindi wa tatu imecheza dhidi ya timu ya taifa ya Lesotho na dakika 90 zikamaliza kwa sare tasa (0-0) kutokana na timu hizo kutoshana nguvu na kila moja kufanikiwa kumiliki mpira kwa asilimia 50 ndio mikwaju ya penati ikaamua mshindi. Licha ya Lesotho kuonekana kuwa wazuri kiasi na kufika golini kwa Taifa Stars mara nyingi lakinihawakuwa wazuri katika upigaji penati na wakajikuta wakifungwa kwa penati 4-2, huku kwa upande wa Tanzania Shiza Kichuya ndio alikosa penati, Himid Maoa, Simon Msuva, Abdi Banda na Raphael Alpha wakafunga penati zote.

Ommy Dimpoz ajibu tuhuma za wizi

Msanii Ommy Dimpoz ambaye sasa anatamba na ngoma yake mpya 'Cheche' amefunguka na kuweka wazi tuhuma za yeye kuiba wimbo na kusema hausiki hata kidogo kwani wimbo huo mpya aliandikiwa na kufanyiwa kila kitu na Goodluck Gozbert (Lollipop). Ommy Dimpoz amesema hayo jana kupitia Friday Night Live (FNL) na kusema yeye hapaswi kuhusishwa hata kidogo kwani yeye alifuata utaratibu wote na kupata wimbo huo hivyo mtayarishaji wa muziki Aby Dad pamoja na msanii wake wanapaswa kudeal na Goodluck Gozbert (Lollipop) na si yeye kwani yeye ataendelea kuipa nguvu kazi hiyo sababu tayari ameshawekeza. "Lollipop alisikilizisha chorus hiyo ya Cheche nikaipenda ila akaniambia wimbo huu haujakamilika, baada ya hapo aliutengeneza wimbo ule mwanzo mwisho kwa kuweka sauti zake mimi nilichofanya ni kufuatisha kile ambacho yeye amefanya, sijaandika chochote, wala kutunga melody wala chochote kile" alisema Ommy Dimpoz Ommy Dimpoz aliendelea kusimulia kuwa "Sasa baada ya

Umesikia alichokisema Alikiba kuhusu Niyonzima?

Mkali wa Bongofleva Ali Kiba ni shabiki mkubwa Yanga na huwa hajifichi katika hilo huku mara kahaa akionekana uwanjani kuisapoti timu yake inapokuwa inacheza mechi mbalimbali. Mbali na ushabiki wake wa Yanga, Ali Kiba na kiungo Haruna Niyonzima ni washkaji sana. Sasa Niyonzima ameondoka Yanga na haijafahamika hadi sasa anaelekea wapi ingawa anahusishwa kujiunga na Simba. Kiba anazungumzia anavyojisikia baada ya uongozi wa Yanga kutangaza rasmi kwamba Niyonzima hata kuwa miongoni mwa wachezaji wao kuanzia msimu ujao. “Nimejisikia vibaya kwa sababu mimi ni shabiki wa Yanga namkubali Niyonzima, lakini mpira ni kazi yake unapokuwa unatumikia sehemu kwa muda mrefu inafika kipindi unataka kwenda sehemu nyingine.” “Kwanza ni historia nzuri kwake kwenye mpira kwamba amecheza klabu fulani na fulani, anatajwa kwenda Simba, ni klabu kubwa vilevile.” “Nitaendelea kum-support kama mshkaji wangu lakini mimi ni shabiki wa Yanga na sija-mind yeye kutoka Yanga kwa sababu ni moja y

Hivi ndivyo Whatsapp ilivyoweza kumaliza tatizo la vikao vya harusi

Dar es Salaam. Je, unataka kuwaunganisha watu kwa urahisi katika maandalizi ya harusi yako au shughuli nyingine yoyote? Jibu ni rahisi na huenda tayari umefanya hivyo. Mtandao wa kijamii wa mawasiliano wa simu ya mkononi wa WhatsApp umekuwa suluhisho la mambo mengi. Aina hiyo ya mawasiliano ambayo huunganisha watu wenye malengo yanayofanana, familia, sehemu za kazi, vyuoni au sehemu za ibada sasa yamekuwa msaada mkubwa nchini. Sehemu mmojawapo ambayo imerahisishwa ni vikao vya harusi ambavyo havihitaji tena watu kwenda kukutana ukumbini au baa, badala yake mambo yote kama kuahidi michango humalizwa kupitia WhatsApp. Na hakuna siri tena kwa kuwa safari za kwenda kwenye baa au hoteli kila Jumamosi na Jumapili kwa ajili ya vikao zimepungua kutokana na shughuli hiyo kufanyika kwenye WhatsApp. Pamoja na harusi, shughuli nyingine zinazofanyika kwa njia hiyo ni pamoja na taarifa za masoko, mikutano ya wanachama wa vicoba na saccos. Shughuli nyingine ni vikao vya ukoo na